BITEKO AWATAKA WANANCHI KUCHANGIA MIRADI YA MAENDELEO




Mbunge wa Jimbo la Bukombe mkoani Geita, Doto Biteko amewataka wananchi wa Kata ya Namonge Wilaya ya Bukombe kuwa mstari wa mbele kuchangia miradi ya maendeleo.
 
Biteko aliyasema hayo wakati akihutubia wananchi wa kata ya Namonge kwenye mkutano wa hadhara akitoa mchango wa mifuko 200 ya saruji yenye thamani ya Tsh milioni 3.7 itakayo saidia ukamilishaji wa ujenzi wa Kituo cha Afya na choo kwa ajili ya wagonjwa.
Biteko aliwataka viongozi wa kamati ya maendeleo ya kata kusimamia kikamilifu ili mradi ukamilike mwaka huu na kuondoa changamoto ya wakazi wa kata hiyo kutembea umbari mrefu wa kilomita 12 toka Namonge hadi kata ya Uyovu kwa ajili ya kufuata huduma.

 
Wakati huo huo Mbunge Biteko ametoa mifuko 78 ya saruji yenye thamani ya sh 1.4 milioni na mabati 10 yenye thamani ya sh 200,000 shule ya msingi Namonge kwenye ujenzi wa Choo cha wanafunzi matundu 20.
Diwani wa Kata ya Namonge Mhe. Mulalu Bundala alisema wananchi wamekuwa wakitembea umbari mrefu kutafuta huduma za Afya na mradi ulianza 2013 malengo ya kukamilika ni mwaka 2019 mradi mpaka sasa umegharimu sh 52 milioni huku nguvu za wananchi sh 8 milioni.

Mkuu wa shule ya msingi Namonge Jemes Masumu alisema ujenzi wa choo hadi kukamilika utagharimu sh 11.3 milioni lakini msada wa mbunge wa mifuko 78 ya saruji itakamilisha mradi huo na kwamba fedha nyingine imetolewa na halmashauri na wadau wa maendeleo.

Masumu alisema choo cha wanafunzi kilititia Mei 3 mwaka 2019 shule hiyo inawanafunzi 3315 wavulana 1644 wasichana 1671 wanajisaidia kwenye choo cha matundu sita ambacho hakikidhi mahitaji wengine kulazimika kutumia choo cha muda kilichozungushiwa nyasi.

 
  


Comments