RUNZEWE ACADEMY FC YAILISHA BAO 2-0 NAMPANGWE

Timu ya runzewe academy fc ya kata ya Uyovu imeilisha bao 2-0 timu ya Nampagwe fc ambayo ilikuwa bingwa wa kata ya Runzewe magaribi katika mchuwano uliofanyika katika uwanja wa Uyovu kutafuta timu itakayo ingia fainali kusaka bingwa wa tarafa ya Siloka mashindano ya ligi ya Doto Cup 2019.
Wafungaji wa magoli ya timu ya Runzewe adademy Mathayo Jeremia dakika ya 20 na goli la pili lilifungwa na Magazi Doto dakika ya 64 hadi kipenga cha mwisho cha mwamzi Nampagwe fc hawakufunga na kuwafanya kutoka kwenye mashindano hayo.
Katibu mkuu wa chama cha mpira wa minguu wilaya ya Bukombe (BUFA) Bosco Mwidadi amesema katika mashindano ambayo  yalikuwa bado yanaendelea huku tarafa zingine zime maliza muzunguko mapema wiki hii.
Mwidadi alisema fainali ya kusaka bingwa tarafa ya siloka itachezwa katika uwanja huo Agost 7 na timu ya Namsega fc na Runzewe Academy  sikuhiyo itaenda sambaba na kukutanisha na timu za Chuif  na  Bukombe Star kutafuta bingwa wa tarafa ya Bukombe mchuwano huo utafanyika uwanja wa Bukombe.
Agost 5 mwaka huu katika viwanja viwili tofauti tarafa ya Ushirombo na tarafa ya kimichezo Bulega  zitakutanisha  timu nne kusaka bingwa kila tarafa ambapo timu ya Nsagali fc ambaye nibigwa wakata ya Ng’anzo itakutana na Sinamila fc bingwa wa kata ya Butinzya katika uwanja wa Bulega timu ya Ushirombo Worrios bigwa wa kata ya Bulangwa itachuwana na timu ya Kilimahewa fc bigwa wa kata ya Katente katika uwanja wa Ushirombo mjini.

Comments