KILIMAHEWA YATWAA UBINGWA WA DOTO CUP 2019






 
















Waziri wa Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu Mhe.

Jenista Mhagama 










       
TIMU ya Kilimahewa fc ya kata ya Katente tarafa ya Ushirombo wilaya ya Bukombe mkoa wa Geita, imetwaa kwa mara ya kwanza ubingwa wa ligi ya Doto Cup 2019 kwa kuichapa timu ya Runzewe Academy goli 2-1 katika faina iliyofanyika katika uwanja wa kilimahewa.

Mfungaji wa magoli ya timu ya Kilimahewa fc Fc  Hamis Julius aliwanyanyua mashabiki wake baada ya kuingiza kimiani bao la kwanza dakika ya 62 na dakika ya 67 aliongeza bao lingine hadi ambali lilidumu hadi kipenga cha mwisho.

Mfungaji wa goli la timu ya Runzewe Academy lilifungwa na Rashidi Sanga dakika ya 13 ambalo lilidumu na kuwa la kufutia machozi timu hiyo ilisha wahi kuchukuwa ubingwa wa Doto Cup misimu miwili 2016 na 2017 mwaka 2018 kombe hili lilichukuliwa na timu Ushirombo Rengezi  2019 limebaki mjini tena Kilimahewa fc.


Mdhamini  wa mashindano bunge wa Jimbo la Bukombe pia waziri wa Madini Doto Biteko katika hafla ya kukabidhi zawadi za washindi aliwasii vijana wa timu 165 zilizoshiriki  katika mashindano hayo yaliyozinduliwa Julai 5 mwaka huu na kufika tamati Agosti 24 kuhakikisha kuwa wanaendeleza vipaji vyao  vilivyoibuliwa na kutumia fursa hiyo kupata ajira.

“Kupitia ligi hii timu zilizoshiriki ni 165 walioshinda na walioshinda wote muwe wamoja katika kuendeleza  urafiki   na vipaji  ambavyo  niajira,” Alisema Biteko.

Mgeni rasmi Waziri wa nchi, ofisi ya Waziri mkuu, (sera, Bunge, kazi, ajira na wenye ulemavu) Jenista Mhagama alisema kuwa iwapo vijana watafuata kanuni, taratibu na sheria za mpira wa miguu kazi hiyo ni ajira rasmi siyo ya kubezwa.

Mhagama licha ya kumpongeza Mbunge Biteko alisema kuwa ligi hiyo ya Doto Cup kama itaendelezwa vijana wanaweza kuepukana na vishawishi vya kujiunga na makundi mabaya kama ya uvutaji wa madawa ya kulevya hali ambayo itapelekea kupata magonjwa mengine ya kuambukiza kama UKIMWI.

Katika hafla hiyo pia  Mhagama aliweza kukabidhi zawadi kwa mshindi wa kwanza Kilimahewa Fc kiasi cha shilingi Milioni 1, mipira mitatu na jeshi seti tatu huku mshindi wa pili ambaye ni Runzewe Academy alikabidhiwa shilingi 500,000, mipila miwili na jezi seti mbili na mshindi wa tatu Sinamila FC alikabidhiwa shilingi 200,000 na mpira mmoja huku Chui Fc mambaye ni mshindi wa nne aliambulia seti moja ya jezi na mpira mmoja.

Kauri mbiu ya ligi hiyo ilikuwa ni “Kusema na kutenda.

Comments