Katibu wa Nec siasa na uhusiano wa kimataifa
CCM Kanali Ngemela Lubinga akizungumza na viongozi wa ccm kuanzia ngazi ya Matawi hadi Wilaya-Bukombe.
Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Bukombe Daniel Machongo akizungumzana viongozi wa ccm kuanzia ngazi ya Matawi hadi Wilaya-Bukombe.
Mbunge Wa Jimbo la Bukombe Mhe.Doto Mashaka Biteko akizungumza na viongozi wa ccm kuanzia ngazi ya Matawi hadi Wilaya-Bukombe.
Mbunge Wa Jimbo la Bukombe Mhe.Doto Mashaka Biteko akiwa ameshikilia cheti cha pongezi kutoka kwa uongozi wa CCM Wilaya-Bukombe na kukabidhiwa na Katibu wa Nec Siasa na Uhusiano wa Kimataifa CCM Kanali Ngemela Lubinga
Viongozi wa Dini na Wazee maarufu wakiwa ukumbini.
Katibu wa Nec siasa na uhusiano wa kimataifa CCM Kanali Ngemela Lubinga amewataka viongozi wa chama cha mapinduzi CCM kuanzia ngazi ya matawi kuhakikisha wanahamasisha wananchi kujiandikisha kwenye daftari la wapiga kura ili waweze kushiriki kikamilifu kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa ikiwa zoezi hilo linatalajiwa kuanza uboreshaji huo Agost 26 serikali inaanza kuboresha daftari hilo ili wananchi waliofikia umri wa miana 18 wawe na haki ya kuchagua kiongozi wanae mtaka.
Katibu wa Nec siasa na uhusiano wa kimataifa CCM Kanali Ngemela Lubinga amewataka viongozi wa chama cha mapinduzi CCM kuanzia ngazi ya matawi kuhakikisha wanahamasisha wananchi kujiandikisha kwenye daftari la wapiga kura ili waweze kushiriki kikamilifu kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa ikiwa zoezi hilo linatalajiwa kuanza uboreshaji huo Agost 26 serikali inaanza kuboresha daftari hilo ili wananchi waliofikia umri wa miana 18 wawe na haki ya kuchagua kiongozi wanae mtaka.
Lubinga aliyasema hayo wakati
akizungumuza na viongozi wa CCM ngazi ya matawi hadi wilaya kwenye mkutano kwa lengo
la kuimarisha chama uliofanyika Wilayani Bukombe na kuhudhuliwa na viongozi wa Wilaya na Mkoa wa Geita kwa lengo la kupokea maelekezo ya chama ngazi ya Taifa.
Alisema mwaka 2015 Tanzania ilikuwa na vituo vya Afya 115
lakini kwa kutekeleza ilani ya CCM
hadi sasa serikali ya awamu ya
tano kuna vituo vya Afya 353.
Lubinga alisema serikali kila mwezi
inatoa Tsh Bilion 24 kwa ajili ya kuhudumia Elimu
Bure kaptesheni za shule ya
msingi na sekondari kwa huku mikopo chuoni serikali kila mwaka inatowa sh 480 bilioni
kwa ajiri ya mikopo wanafunzi wa chuo naserikali inatalajia kununua ndege
zingine.
Mbuge wa Jimbo la Bukombe Doto Biteko
ambae pia ni Waziri wa Madini aliwaomba viongozi wa chama kuacha makundi badala yake watimize wajibu wa
kuwahudumia wananchi ili washiriki vizuri kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa
zitakazo fanyika Oktoba mwaka huu.
Comments
Post a Comment