DOTO CUP YAZIDI KUSHIKA HATAMU TIMU 6 ZATINGA HATUA YA FAINALI NGAZI YA TARAFA



Timu 6 kati ya nane zinazotarajia kuingia hatua ya fainali ngazi ya Tarafa katika Mashindamo ya Mpira wa Mguu kombe la Dotto Cup 2019 wilaya ya Bukombe mkoani Geita zimefuzi kuingia katika hatua hiyo baada ya kuibuka na ushindi kwenye hatua ya mashindano ngazi ya tarafa.

Mashindano hayo yalianza kutimua vumbi Julai 8, mwaka huu yakishirikisha jumla ya Timu 165 kutoka ngazi ya kijiji na jumla ya Timu 17 ziliingia katika hatua ya fainali ngazi ya Tarafa.

Ligi hiyo imeingia hatua ya fainali ngazi ya Tarafa na kwamba kwa mujibu wa Katibu Mkuu wa Chama cha Mpira wa Miguu wilaya ya Bukombe (BUFA) Bosco Mwidadi timu zilizofuzu kuingia hatua hiyo baada ya michezo Minne iliyofanyika katika Viwanja vya Ushorobo kati ya Timu ya Kilimahewa FC iliyoibuka na ushindi wa Mabao 3-1 dhidi ya wenyeji timu ya Bukombe United.

 Katika Uwanja wa Tarafa ya Bukombe Timu ya Chui FC imeichapa 3-1 Timu ya Iyogelo FC,Uwanja wa Uyovu Timu ya Namonge FC imeibuka na ushidi wa bao 1-0 dhidi ya Namsega FC,na katika Tarafa ya Kisoka Timu ya Sinamila FC imeibuka na Ushidi wa mabao 2-0 dhidi ya Miyenze FC.

 Mwidadi amezitaja timu ambazo zitacheza fainali ngazi ya tarafa Julai 5 mwaka huu kutafuta bingwa kwa kila tarafa ni timu ya NGM FC itakutana na Sinamila fc katika uwanja wa Bulega huku timu ya Bukombe star itakutana na timu ya Chui fc zitacheza katika uwanja wa Bugelenga na timu ya Ushirombo Worrios itachuwana na timu ya Kilimahewa fc uwanja wa Ushirombo mjini katika tarafa ya Siloka bado mashindano  yanaendelea kutafuta timu mbili zitakazo ingia fainali hiyo. 

Mwidadi amesema kwamba mashindano hayo yanadhaminiwa na Mbunge wa Jimbo hilo ambaye ni Waziri wa Madini Doto Biteko lengo likiwa ni kuibua,kuendeleza,na kukuza vipaji vya  soka wilayani hhapa pamoja na kujenga mahusiano mema kwa jamii ya wilaya hiyo.

Fainali ya mashindano hayo inatarajia kufanyika Agosti 10 au 12 ,mwaka huu kwa kutegemea karenda ya mdhamini wa mashindano.


Comments