AHUKUMIWA KWENDA JELA MAISHA BAADA YA KUMBAKA MTOTO WA MIAKA MITATU

Image result for arrest
Mahakama ya Hakimu mkazi Wilaya ya Bukombe Mkoa wa Geita,imemuhukumu kwenda kutumikia adhabu ya kifungo cha maisha jela mkazi wa kijiji cha Lyobahika kata ya Uyovu Tarafa ya Siloka  Ruben Maiko (19) kwa kosa la kumbaka mtoto wa umri wa miaka mitatu.
Hakimu mkazi Mahakama ya Wilaya ya Bukombe Amon Kahimba akitoa hukumu hiyo alisema mshtakiwa alitenda kosa la ubakaji majira ya saa 1:00 jioni Agosti 8 mwaka 2019  kijiji cha Lyobahika akiwa nyumbani  kwa  Doto Wiliamu anaedaiwa kuwa mpenzi wake na mama wa mtoto aliye bakwa.
Mshtakiwa aliingia chumbani akamuita mtoto chumbani na kumbaka kisha kumusababishia maumivu makali sehemu ya  mwili wake baada ya kumkuta mama wa mtoto huyo hayupo ameenda kwenye majukumu yake.
Kahimba alisema kutokana na ushahidi uliotolewa na upande wa mashitaka mahakamani hapa na vielelezo vya madaktari na upande wa Doto Wiliamu mama mzazi wa mtoto na mashuuda wengine ushahidi ambao hauja acha shaka mahakamani.
Kutokana na kosa hilo mshtakiwa ataenda kutumikia kifungo cha maisha jela ili liwe fundisho kwa watu wengine wenye nia ovu ya kutenda kosa kama hilo.
Mshitakiwa Ruben Mariko akitowa utetezi wake mahakamani hapo aliomba mahakama kumpunguzia adhabu kwa kutoisumbua alikili kutenda kosa hilo na kuongeza kuwa alikuwa na mahusiano ya kimapenzi na mama wa mtoto huyo alifika nyumbani hapo akamkuta mpenzi wake amekwenda kuhudumia bar ndipo akambaka mtoto wa mpenzi wake.
Awali mwendesha mashtaka wa polisi Neema Nhaluke aliomba mahakama kutowa adhabu kali kwa mshtakiwa kutokana na vitendo vya kubakwa watoto  vimekuwa vikitokea mara kwa mara Wilayani hapa.

Comments