SMALL TIGER FC YATWA UBINGWA DOTO CUP KWA KATA YA LYAMBANGONGO




Timu ya Small Tiger Fc ya Lyambamgongo imeibuka kidedea kwenye Lingi ya Doto Cup 2019 ngazi ya Kata baada ya kuilaza timu ya Kagwe fc kwa goli 3-2.
Wafungaji wa magoli ya Small Tiger Fc John Nyahiti dakika ya 15 na Greyson Mtingwa kufunga magoli mawili dakika ya 42 na ya 52.
Magoli ya timu ya Kagwe fc yalifungwa na Kashinje Joseph dakika ya 10 na Mathias Charles dakika ya 36.

Aidha Diwani wa Kata ya Lyambamgongo Boniphance Shitobelo ambae alikuwa mgeni rasmi katika kukabidhi zawadi za washindi wa kata hiyo ambazo ni seti moja ya jezi na mpira mmoja kwa mshindi wa kwanza,  mshindi wa pili Kagwe fc walipewa mpira mmoja.

Shitobelo akikabizi zawadi alisema katika kata hiyo kulikuwa na timu nne zilizoshiriki katika mashindano hayo Small tiger fc, Ifunde fc, Kagwe fc na Ishololo fc ikiwa timu iliyo shinda ngazi ya Kata ni Small tiger fc na ushindi huo itaenda kukutana na timu nne mabingwa wa Kata zingine ngazi ya Tarafa ya Bukombe.

Shitobelo aliwataka wachezaji kuwa na ushirikiano na timu zilizo shindwa ilikuongeza nguvu na kutwaa ubingwa kwa ngazi inayofuata

Kwa upande wake nahodha wa Timu ya Small Tiger Fc John Nyahiti alianza kwa kumshukuru Mbunge wa Jimbo la Bukombe Doto Mashaka Biteko kwa uamuzi wake wa kuwaunganisha vijana ki michezo na kuwashukuru wachezaji wenzake kwa kuwa na ushirikiano hadi wameibuka mabibwa wa Kata huku wakiwahahakishia mashabiki wao kutwaa ubingwa wa Doto cup 2019 katika ngazi ya Wilaya naye nohodha wa timu ya Kagwe fc Ngusa Sameke alisema mchezo ulikuwa mzuri na kwamba haya matoke wameyapokea vyema.

Katika kiwanja cha michezo Kata ya Iyogelo kwa mjibu wa msimamizi wa fainali ngazi ya Kata Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Miguu Mkoa wa Geita (GEREFA) Joseph Kabote alisema Timu zilizoshiriki kwenye Kata hiyo ni  Iyogelo Fc, Shibingo Fc, Bugando Fc, Nyamakunkwa Fc.

Kabote alisema katika fainali hiyo timu ya Iyogelo Fc imeibuka bigwa wa Kata baada ya kuichapa timu ya Shibigo Fc goli 9-8 huku timu hizo mbili zilicheza na kutoka sale ya moja kwa moja na kuingia kutega matuta.



Comments