RAIS MAGUFULI AMPONDA KIAINA WA JINA WAKE 'JOHN' KWA UZEMBE KUZALISHA


Rais wa Tanzania, John Magufuli amesema tangu kuanzishwa kwa kikosi kazi cha kupambana na ujangili mwaka 2016 idadi ya wanyama hapa nchini imeongezeka.
Magufuli amesema hayo leo Jumanne Julai 9 mwaka 2019 wakati wa uzinduzi wa Hifadhi ya Taifa ya Burigi-Chato mkoani Geita.
"Mwaka 2014 kulikuwa kuna tembo 43,330 lakini hivi sasa baada ya kuanzisha kikosi cha kupambana na ujangili wamefikia zaidi ya 60,000 faru hawakuwepo kabisa ila sasa wamefikia 163 hatuna budi kumshukuru Faru Rajabu mtoto wa Faru John," amesema Magufuli.
"Inaonekana yule Faru wajina wangu (John alikuwa hajitumi vizuri) huyu mtoto wake nimeambiwa mpaka sasa amekwisha zalisha 43," amesema Rais Magufuli huku akitabasamu.

Comments