MAPINDUZI FC YAICHAPA 3-1 KADIS FC (Doto cup 2019)

Michuano ikiwa inaendelea kati ya Mapinduzi Fc Vs Kadis Fc katika viwanja vya shule ya msingi igulwa

Timu ya Mapinduzi fc ya Katente imeichapa magori 3-1 timu ya Kadis fc ya bomani katika michezo ya lingi ya Doto Cup 2019 uwanja wa shule ya msingi Igulwa kata ya Katente wilaya ya Bukombe mkoa wa Geita.
Mchezaji wa timu ya mapinduzi fc Aron Peter alijifunga goli moja dakika ya 22 baada ya muda mchache kupachika gori timu ya Kadis fc dakika ya 13 huku goli lapili timu ya Mapinduzi fc lilifungwa na Mathew Mabenga dakika ya 54 goli la tatu lilifungwa na Salumu Salum dakika ya 58.
Mchezaji wa timu ya Kadis fc Maganga Paschal alipewa kati nyekundu kwa kosa la kumudanganya mwamzi wa mchezo huo Projestus Luta kuwa ameumia akigalagala chini kwa kupoteza muda huku akiwa na kadi ya njano.



Luta alisema kwa sheria za mpira wa miguu mchezaji huyo haluhusiwi kucheza mechi tatu atakuwa ndani ya adhabu.
Mchezaji huyo Maganga Paschal akizungumzia kupewa kadi nyekundu alisema hakuwa na talajio ya kupewa kadi nyekundu na hakufanya kosa kwamakusudi kunakitu kilimfanya kulala kutokana na kuumia  gafra.
Alisema hakuna namuna atatumikia adhabu aliyopewa anaiombea timu yake isitolewe kwenye michezo miwili iliyoko mbele ili ajumwike nao kuhakikisha wanatafuta ushindi wa kwanza kati ya timu zinazoshiriki mashindano ya Doto Cup
.

 
Mkazi wa Katente Lazaro Machibya alimpongeza mbunge wa jimbo la Bukombe Doto Biteko kwa kudhamini mashindano ya mpira wa miguu kila mwaka hali ambayo imekuwa ikiwafanya wapenzi wa michezo kufurahi kutokana na kutokuwepo mashindano mala kwa mala ya mpira wa miguu.

Comments