Ikiwa ni mwendelezo wa
michuano ya Doto Cup 2019 Timu ya Makirikiri Fc ya Ikuzi Kata ya Runzewe
Mashariki Wilaya ya Bukombe Mkoa wa Geita, imetwa ubingwa ngazi ya Kata katika
mashindano ya fainali ligi ya Doto Cup 2019 kwa kuichapa timu ya Nampangwe fc
goli 2-1.
Magori ya timu ya
Makirikiri Fc yaliwekwa wavuni na Vitina Kabili
dakika ya 11 na dakika ya 50
Na mfungaji wa gori la
Nampangwe fc lilifungwa na Bundala Heriman dakika ya 84.
Katika mchezo huo Pia nahodha
wa timu ya Nampangwe Mawazo Yohana
amesema kuwa matokeo ya kushindwa wameyapokea na kwamba ni matokeo ya mchezo.
Yohana aliwaomba
wachezaji wa timu ya Makirikiri fc kuendelea kuwa na ushirikiano ili wachukuwe
ubingwa wa Tarafa ya Siloka.
Upande wake nahodha wa
timu ya Makilikili fc Jeoseph Lucas amesema wamefikia ushindi huo na kutwa
ubingwa wa kata kutokana na ushirikiano
na kujituma wachezaji.
Diwani Viti Malumu Kata
ya Runzewe Mashariki Mary Nchiba akikabidhi zawadi na Diwani wa Kata ya Runzewe
Mashariki Maduhu Mwanambati wamesema katika Kata hiyo zilikuwa zimeshiriki timu
8 lakini Makirikiri Fc imetwaa ubingwa wa Kata hiyo.
Nchiba alimpongeza
Mbunge wa Jimbo la Bukombe Doto Mashaka Biteko kwa kudhamini mashindano kila
mwaka ili kuibuwa vipaji kwa vijana na kuwajengea Afya.
Makirikiri fc
imejinyakulia Zawadi ya ubingwa wa Kata seti moja ya jezi na mpira mmoja huku
mshindi wa pili Nampangwe fc walipewa mpira mmoja.
Comments
Post a Comment