Mashindano ya Doto Cup 2019 ngazi ya
tarafa yakiendelea kushika kasi timu ya Kilimahewa fc toka kata ya Katente
imeichapa goli timu ya Bukombe united toka kata ya Igulwa goli 3-1.
Wafugaji wa timu ya Kilimahewa fc
Musa Moja dakika ya 10 Juma Nela dakia ya 25 Mbagara Koster dakikaya 98 huku
mfungaji wa goli la timu ya Bukombe United Juma Richard dakia ya 66 kupitia
mkwaju wa Penaliti.
Kwa mjibu wa katibu wa chama cha
mpira wa miguu wilaya ya Bukombe (BUFA) Bosco Mwidadi amesema katika Uwanja wa
Tarafa ya Bukombe Timu ya Chui FC imeichapa 3-1 Timu ya Iyogelo FC,Uwanja wa
Uyovu Timu ya Namonge FC imeibuka na ushidi wa bao 1-0 dhidi ya Namsega FC,na
katika Tarafa ya Kisoka Timu ya Sinamila FC imeibuka na Ushidi wa mabao 2-0
dhidi ya Miyenze FC.
Kocha wa timu ya Bukombe United Musa
Mzunzu amesema matokeo hayo ameyapokea na kwamba mchezo unamatokeo matatu
kushindwa kushinda na sale.
Huku kocha wa timu ya Kilimahewa fc Joseph
Kapelo amesema wameshinda kutokana na makosa ya timu ya Bukombe united na
kwamba kikosi chake kiko safi atahakikisha ana twa ubigwa wa tarafa.
Comments
Post a Comment