Diwani wa Kata ya Bulangwa Wilaya ya Bukombe Mkoa wa
Geita, Yusuph Mohamed amewaomba Wananchi wa Kata hiyo kushiriki kwenye miradi ya
maendeleo kwa kujitolea kuchimba msingi na kusongeza mawe, mchanga, na kusomba
maji ya kujengea.
Mohamed alitowa wito huo wakati akiwashukru wananchi kuja
kujitolea kuchimba msingi wa mradi wa ujenzi wa Zahanati katika kijiji cha
Bulangwa.

Alisema katika nguvu za wananchi Mbunge wa Jimbo la Bukombe
Mhe. Doto Mashaka Biteko amechagia sh milioni 6 kwa ajili ya kununua mifuko 250 ya simenti
na kusomba mchanga na mawe.

Kwa upande wake Mwenyekiti
wa Kijiji cha Bulangwa Amos Manumbu amesema mwaka 1999 Kijiji kiliazishwa wananchi na tangu
kipindi hicho wamekuwa wakifuata huduma za Afya katika Kituo cha Ushirombo.
Manumbu
alisema kutokuwa na Zahanati kijijini hapo ni changamoto kubwa kwa wananchi hasa wanawake
wenye ujauzito hali ambayo inayowafanya wengine kutohuzuria kliniki ya mama
baba na mtoto.
Mkazi wa kijiji cha Bulangwa Bundala Migayo aliomba serikali iwaunge mkono wananchi ili waondokane na changamoto ya kutembea umbali mrefu kutafuta huduma ya Afya.
Mkazi wa kijiji cha Bulangwa Bundala Migayo aliomba serikali iwaunge mkono wananchi ili waondokane na changamoto ya kutembea umbali mrefu kutafuta huduma ya Afya.
Kaimu Mhandisi wa Ujenzi Wilaya ya Bukombe Dominico Shilingo alisema ujenzi wa Zahanati ya Bulangwa itakamilika kwa mjibu wa mkataba siku 90 hadi kukamilika na itaghalimu Tsh milioni 68 .
Comments
Post a Comment