BITEKO AKABIDHI VIFAA TIBA VYENYE THAMANI YA MILIONI 56 BUKOMBE






 



Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mkoani Geita Mhe. Doto Mashaka Biteko amekabidhi vifaa tiba vyenye thamani ya Tsh milioni 56 katika Hospitali ya Wilaya ya Bukombe. 

 Miongoni mwa vifaa tiba hivyo ni vitanda kwa ajili ya upasuaji na vingine wodini na baiskeli za wagonjwa na fimbo za kutembelea wazee. 

Biteko ambae pia ni Waziri wa Madini aliushukuru uongozi wa Shdepha+ Kahama kwa msaada wao ikiwa ugonjwa wa kifua kikuu ni mbaya na pia serikali inabeba mzingo mkubwa wa kutoa matibabu bure.

Waziri wa Madini Biteko alitoa wito kwa Watanzania wote wanaojishughulisha na uchimbaji madini kuchukua tahadhali ya kujikinga na maabukidhi ya kifua kikuu.

Mkurugenzi wa miradi ya Shdepha+ Kahama Venancy Kabwebwe akikabidhi msaada wa piki piki na bajaji alisema kuunga mkono serikali ilivyo boresha sekta ya afya kwa kujenga zahanati na kuongeza bajeti kitaifa shdepa imetowa msada wa na Bajaji zenye thamani ya sh 240 milioni.

Kabwebwe  alisema katika Mkoa wa Geita Wilaya ya Bukombe imepewa kipaumbele kutokana na wilaya hiyo imeathilika sana na ugonjwa wa kifua kikuu.

Alisema Wilaya imeathilika hasa maeneo ya migodini na vijiji ambako huduma za upimaji  hazitolewi vizuri pikipiki hizo na bajaji zitakusanya makohozi nyumba kwa nyumba na migodini na kukimbiza kwenye maabara ya hospitali ya Wilaya na kurudisha majibu ili kutoa matibabu kwa wagonjwa.

Mratibu wa ugonjwa wa kifua kikuu Wilaya ya Bukombe Dk Joshua Mazingo alisema Wilaya ya Bukombe kimkoa inaongoza kuwa na wagonjwa wengi wa kifua kikuu.
"Vifaa hivi vitasaidia kuboresha huduma za afya na kuhakikisha wanakusanya makohozi ya watu wanapopimwa katika vituo vya afya na zahanati kwa wakati"  Alisema Mazingo.

 Akipokea vifaa hivyo kwa niaba ya Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bukombe Katibu wa Hosptali ya wilaya amesema wamepokea  msaada wa pikipiki tano,Bajaji mbili toka shirika la Shdepha+ Kahama kwa ajili ya kitengo cha Kifua kikuu sanjari na vifaa tiba ambavyo ni vitandakwa ajili ya upasuaji ,baiskeli za wagojwa na fimbo za kutembelea wazee kutoka kwa Mbunge Jimbo la Bukombe  Mhe. Doto Mashaka Biteko.
 Mkuu wa Wilaya ya Bukombe Said Nkumba aliwataka waunguzi na madaktari kutunza vifaa vilivyo letwa na wadau wa maendeleo akiwemo mbunge ili visaidie wananchi.

Comments