SERIKALI YATOA MASAA 84 KWA MAKAMPUNI YA KUNUNUA PAMBA

Mkuu wa Wilaya ya Bukombe Said Nkumba akizungumza Katika kikao cha Baraza la Madiwani Wilayani Bukombe

Bukombe,Serikali imetoa masaa 84 kwenye makampuni manne yaliyofunga mkataba wa kununua zao la pamba wilayani Bukombe mkoani Geita wawe wameanza kununua pamba hiyo.
Tamko hilo la serikali lilitolewa na mkuu wa wilaya ya Bukombe mkoani Geita, Said Nkumba saa 9:58 alasili juni 20 mwaka huu kwenye kikao cha baraza la madiwani halmashauri ya wilaya ya Bukombe.
Nkumba alimuagiza mkaguzi wa pamba wilaya ya Bukombe Edmond Jemes kuhakikisha itakapo fika saa 8:00 mchana Juni 24 kama kutakuwa na kampuni ya kununua pamba halija fika kwenye kituo apate taarifa ili achukuwe hatua.
Alisema kwenye taarifa za madiwani Juni 19 wakati wakiwasilisha taarifa za utekelezaji wa shughuri za maendeleo na changamoto za wakulima walidai baadhi ya wakulima wameaza kutorosha zao hilo na kwenda kuuzia wilaya jirani na halmashauri inakosa mapato.
Bazi ya makampuni matatu mameneja walifika kujibu na kutoa sababu zilizo chelewesha kunaza kununu pamba Furesho, KCCL na Kahama oil mili, huku inadaiwa kuna makampuni manne yaliyofunga mkataba kununu pamba wilaya ya Bukombe yote matawi ya Kahama.
Meneja wa kampuni Furesho Kifashizi Ngalula akiwa kwenye baraza alisema bei ya sh 1200 ilikuwa inawakata na kampuni inatalajia kufungua vituo vya kununuria pamba jumatatu kilichowasababisha kuchelewa kuanza ununuzi ni kutokana na kushuka kwa bei ya pamba soko la duniaanaishukuru serikali imesha kaa na wadau na wamekubaliana kuanza kununua pamba.
Meneja wa kampuni ya KCCL Edward Lubacha akijitetea kwenye baraza  alisema tangu Mei 2 walisuwa suwa kuanza kununu kwa  kupolomoka kwa bei ya kidunia na kwamba kampuni linatalajia kuwa na vituo 46 za kununulia pamba wilayani Bukombe.
Meneja wa kampuni ya  Kahama oil mili Amos Ndutu aliliambia baraza la madiwani kuwa jumatatu kampuni ita anza kununua imeingia na mkataba na vyama vya msingi 47 walichelewa kuanza kutokana na  kushuka kwa bei ya soko la pamba kidunia lakini kwa sasa serikali imefikia muafaka na wakurugenzi wa makampuni.
Upandewake mkaguzi wa pamba wilaya ya Bukombe Edmond Jemes akipokea maelekezo ya serikali yaliyotolewa na mkuu wa wilaya hiyo aliwahakikishia madiwani kuwa makampuni yameelekezwa kuto shusha bei ya sh 1200 kwa kilo moja.
Jemes alisema nikweli kwamba bei ya pamba kidunia ilikuwa imeshuka hadi kufikia sent paund 75 na imeendelea kupolomoka hadi sasa ni senti 67 sawa na sh 1060 ya kitanzania na Mei 1 msimamo wa serikali ilikuwa makampuni wanunuwe kwa sh 1200 kwa kilo na hata sasa serikali imeelekeza waingie sokoni kwa bei ya sh 1200 kwa kilo na hakuna kukopa pamba kwa wakulima.
Mwenyekiti wa halmashauri Safari Mayala alisema kwa maangizo ya mkuu wa wilaya kama halmashauri watayafanyia kazi na kampuni ambayo itakuwa haija ingia sokoni kununua pamba serikali ya wilaya ya Bukombe itafuta mkataba na kampuni ambalo halita tekeleza angizo la serikali ili halmashauri itafute makampuni mengine ispoteze mapato.

Comments