SERIKALI IMEWATAKA VIJANA KUWA NA MSHIKAMANO ILI KUJIKWAMUA KIUCHUMI


Mkuu wa Wilaya ya Bukombe Said Nkumba akizungumza na vijana waliohudhuria semina ya kitalu nyumba Wilayani Bukombe

           
Serikali imewaka vijana kuwanaushirikiano wanapokuwa wanafanya shughuli za uzalishaji wa mali kwa lengo la kujikwamua na umaskini.
Wito huo ulitolewa na mkuu wa wilaya ya Bukombe Said Nkumba wakati akifungua mafunzo ya siku nane vijana 100 mafunzo yanayolenga kuhudumia mazo ya bustani kwa kutumia teknolojia ya kitalu nyumba kata ya Bulangwa wilaya ya Bukombe  mkoa wa Geita.

Nkumba alisema serikali imetowa sh 13 milioni toka ofisi ya waziri mkuu kwa vijana wilaya ya Bukombe ili wanufaike na kilimo cha kitalu nyumba.
Aliwataka vijana baada ya mafunzo haya wawe na hamasa ya kuendelea kulima kiliomo chakitalu nyumba kwa kuzingatia mafunzo na teknolojia wanayopewa.
Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Bukombe Dioniz Myinga aliwaomba vijana ambao wamekuja kujifunza mafunzo hayo kuwa chachu ya maendele kwenye vijiji ili mradi huu ufike kila kijiji.
Myinga alisema kilimo cha kitalu nyumba kitawapa ajila ya kujiajiri vijana na kukuza uchumi kuanzia ngazi ya familia na taifa.
Mtalamu wa kuchanganya udongo na upandaji mazao ya bustani kwa kutumia teknolojia Joseph Athanas toka kampuni ya Holygrnee agric limited iliyopo mkoani Morogoro (vijana sua) ambaye pia muwezeshaji wa mafunzo hayo.

Athanas alisema kampuni hii imepewa tenda na serikali kupitia ofisi ya waziri mkuu kutowa mafunzo kwa vijana 100 kila wilaya hapa nchini kwa kushirikisha vijana wa malika yote hadi umri wa miaka 36 awe amesoma hata kama hajasoma.
Athanas aliongeza kuwa serikali kwa kupitia mafunzo hayo vijana wengi watanufaika badara ya kupitia vikundi vya vijaja na walemavu na wanawake kwa kusubili mkopo wa halmashauri.

Mafunzo haya yatawafanya vijana kujitegemea wao kuendeleza kilomo badara ya kutegemea fedha za halmashauri kupitia mapato ya ndani asilimi 4 ya vijana asilimia 4 ya wanawake asilimia 2 walemavu hali ambayo zimekuwa haziwanufaishi.
Rahery Ernest ambae nimshiriki wa mafunzo alisema wanaishukru serikali kwa kuwaletea mafunzo kupitia mafunzo haya wataenda kuazisha kilimo cha kitalunyuba vijiji ili kuhakikisha vijana wanajikwamua kiuchumi.




Comments