WAZIRI MPINA ATOA ONYO KWA WATUMISHI WANAOKAMATA MIFUGO NA KUISHIKILIA HADI KUFA IKIWA MIKONONI MWAO

Waziri
wa Mifugo na Uvuvi Mhe.Luhaga Mpina amesema serikali itaendelea
kuwachukulia hatua za kisheria watu wanaofanya ukatili kwa wanyama
ambapo amesema ifikapo tarehe 1.Julai ,2019 watendaji wanaoshikilia
mifugo hadi kufa ikiwa mikononi mwao watashughulikiwa.
Mhe.Mpina
amesema hayo leo Mei 22,2019 Bungeni jijini Dodoma ambapo amesema
mifugo ni rasilimali za nchi kama rasilimali nyingine na wizara yake
haitavumilia kuona mtendaji wa Serikali akishikilia mifugo mpaka ina
kufa kwa kigezo cha kufuata sheria kwani hata mifugo nayo ina sheria
zake.
Awali
,Naibu waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe.Abdallah Ulega wakati akijibu
swali la mbunge wa Wa Morogoro Kusini Prosper Mbena aliyehoji juu ya
ukatili wa wanyama kushamiri nchini ,chama cha kuzuia ukatili wa wanyama
Tanzania ,TSPCA kina shirikiana kwa kiasi gani na Serikali ili kuzuia
ukatili ,Mhe.Ulega amezitaja sheria za wanyama pindi wanapokamatwa ikiwa
ni pamoja na kupatiwa malisho,maji na chanjo.
Kuhusu
uanzishwaji wa viwanda vya kuchakata na kusindika nyama katika maeneo
yaliyo karibu na wafugaji ili kupunguza ukatili wa wanyama pindi
wanaporundikwa kwenye magari wakati wanaposafirishwa Kwenda Dar Es
Salaam kwa ajili ya kuchinjwa,Mbunge wa Msalala Ezekiel Maige amehoji
lini serikali itaanzisha viwanda katika maeneo mbalimbali ya wafugaji
nchini ikiwa ni pamoja na Shinyanga.
Naibu
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega amesema mchakato wa kufufua
viwanda vya kuchakata na kusindika nyama nchini upo palepale na
kinachotakiwa ni kupata mwekezaji aliyejipanga vizuri.
Hata hivyo,Serikali inashirikiana na mashirika yasiyo ya kiserikali
kama TSPCA katika kudhibiti vitendo vya kikatili kwa wanyama kwa
kuzingatia sera ya mifugo ya mwaka 2006 na sheria ya Ustawi wa wanyama
ya mwaka 2008 kwa kuelimisha jamii.
Mwaka
2018 jumla ya Makosa 3,542 kwa kosa la ukatili wa wanyama
yaliripotiwa ambapo ni ng’ombe 847 ,mbuzi na kondoo 1,578,nguruwe
88,kuku 539 na punda 490.
Comments
Post a Comment