Top Stories IKULU: Rais Magufuli leo amemteua Mwandishi Mkuu wa Sheria


Leo May 23, 2019 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli amemteua Onorius John Njole kuwa Mwandishi Mkuu wa Sheria (Chief Parliamentary Draftsman – CPD).
Uteuzi wa Njole umeanza leo May 23, 2019.
Kabla ya uteuzi huo, Njole alikuwa Mkurugenzi wa Sheria na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii (SSRA).
Njole anachukua nafasi ya Sara K. Barahomoka ambaye anastaafu.

Comments