Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mkoa wa Geita, Doto Biteko na
Waziri wa Madini amewaomba viongozi wa madhehebu ya dini kuhimiza waumini wao
kusomesha watoto ili kujikomboa na umasikini na kushika nyadhifa mbali mbali za
serikali na chama pamoja na uongozi wa dini.
Biteko alitowa wito huo wakati akihutubia mamia ya waumini wa
kislamu na wakristo baada ya zoezi la kufuturu pamoja katika ukumbi wa Runzewe Sekondari
kata ya Uyovu Tarafa ya Siloka Wilayani Bukombe mkoani hapa.
Alisema ili kuwa na Taifa bora lazima wazazi na walezi Wilaya
ya Bukombe wawekeze kwenye Elimu kwa kushirikiana na viongozi wa madhehebu na
tasisi zingine ikiwa serikali imetowa Elimu bure kuanzia darasa la awali hadi
kidato cha nne.
“Safu iliyoko meza kuu ipo siku watafika ukomo wa uongozi ikiwemo
mimi ili kupata kiongozo bora wanabukombe tuwekeze kwenye Elimu natamani Wakuu
wa Wilaya,Wakuu wa Idara kwenye halmashauri mbali mbali nchini, Mikutano ya Kimataifa
UN”alisema Biteko.
“Na umoja wa afirika
Sadek, na nchi zingine za kiafirika miaka kadhaa inayo kuja wawemo
watoto kutoka Wilaya ya Bukombe inawezekana, inawezekana maadalizi ya mtoto
hayaitaji nafasi au utajili yanaitaji mtoto kutiwa moyo”alisema Biteko.
Kwa upande wake Sheikh wa Mkoa wa Mwanza Hasani Kabeke aliwataka
wasilamu kudunisha amani upendo na kushirikiana na wakristo katika kumuabudu
mungu katika kweli na kuacha matendo ya siyo mpendeza Mungu.
Kabeke alimpongeza Mbunge wa Jimbo la Bukombe tangu
achanguliwe kuwa Mbunge 2015 na 2016 alianza kufuturisha waislamu hadi leo
mwaka wa nne, sheikh alimuomba Mbunge
mwaka wa uchanguzi mkuu 2020 asisite kuanda ftari ya waisilamu na istafasiliwe
ni Rushwa.
Akizungumza kwa niamba ya viongozi wa madhehebu ya ki kristo
Mwenyekiti wa Parokia ya Bikra Maria Msaada wa Daima Ushirombo Daniel
Lutonja alisema mbunge huyu amekuwa
akifanya jambo jema la kuwa na mahusiano ya madhehebu ya dini.
Lutoja aliwaomba wananchi kila mtu kwa imani yake kuendelea
kumuombea mbunge na viongozi wenzake akiwemo Rais John Magufuli kwa kazi kubwa
wanazozifanya.
Mkuu wa Wilaya ya Bukombe Said Nkumba aliwatakia waislam wote
mfungo wa ramadhani mwema na maandalizi mema ya sikuku ya kufungua ambayo kama
haitabadilika karenda itakuwa Juni 4 au Juni 5 mwaka huu.
Nkumba alisema Kamati ya Ulinzi na Usalama Wilaya imejipanga
vema kuhakikisha sherehe za waislamu wanasherekea kwa amani na yeyote atakae
fanya fujo atachukuliwa hatua kali za kisheria.
Comments
Post a Comment