Mkuu wa Mkoa wa Geita, Robart
Gabriel akizungumza na wakazi wa Uyovu Wilayani Bukombe.
Meza kuu wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Geita, Robart
Gabriel
Halmashauri sita zinazounda Mkoa wa Geita, kuanza kujenga masoko ya dhahabu ili wachimbaji wadogo wadogo na wananchi wengine kunufaika na madini ya dhahabu yaliyopo chini ya Ardhi ya Mkoa wa Geita.
Agizo hilo lilitolewa na Mkuu wa Mkoa wa Geita, Robart
Gabriel akiwa kata ya Uyovu Wilayani Bukombe wakati wa ziara ya kwenda
anasikiliza kero za wananchi na kuzitatua.
Alisema kutokana na upatikanaji wa dhahabu katika makusanyo
ya kodi mwaka jana amekusanya sh bilioni 11 toka mgodi mmoja kwa mwaka baada ya
kubana mianya ya rushwa na utoloshaji wa madini.
Gabriel alisema kupitia soko la dhahabu lililofunguliwa mwaka
jana mkoani hapa serikali imepata sh 20 bilioni kutokana na kudhibiti mianya ya
utoloshwaji wa madini.
Na kwamba kuna fedha nyingine sh bilioni 11 iliyopatikana kwa
mwaka jana kutoka mgodi wa GGM kufatia
hali hiyo itanufaika na fedha hizo ikiwemo Bukombe imetengewa sh milioni 100 kwa
ajili ya miradi ya maendeleo ili kubadilisha sura ya Mkoa wa Geita na mei mwaka
huu atafungua soko la dhahabu na kila Wilaya itakuwa na soko la dhahabu.
Aliwataka watumishi wa umma kuwa waadilifu kwa fedha za
serikali ikiwa hapo nyuma Mkoa wa Geita ilikuwa nyuma kutokana na viongozi wa
serikali na watumishi wengine wa chini walikuwa sio waminifu na walipenda
Rushwa.
Miradi ya maendeleo katika idara ya Elimu vyumba vya madarasa
2500 vimekamilika kwa mwaka 2018 na zahanati
wakati anakuja Mkoani hapa kulikuwa na asilimia 25 tu ya miundo mbinu ya zahanati leo kila kijiji kuna maboma na kufikisha asilimia 66.5 uboreshaji wa miundombinu ya afya na ifikapo 2021 hakuna kuzungmuzia upungufu
wa madarasa wala matundu ya vyoo lengo la serikali kusogeza huduma ya Afya kwa
wananchi.
Gabriel alisema uchumi wa Geita unapatikana kutokana na
dhahabu na malengo ya serikali ya Mkoa ni kujenga kijiji cha Uchumi na tayari zimetengwa
hekari 100 na tasimini ya michoro imekamilika baada ya maoyesho ya kitaifa
mwaka huu Dar es Salaam Geita itapokea
watu wa kigeni kwenye maonyesho ya dhahabu kimataifa ikiwa Mkoa wa Geita uko katikati ya Umoja wa Afirika Mashariki.
Samson Jeremia aliipongeza serikali ya Mkoa kwa makusanyo ya
fedha na kwamba serikali itakapo jenga soko la dhahabu Bukombe watanufaika
zaidi.
Juma Yusuph alisema alikuwa hajui kama Geita inautajili
aliomba serikali kubadilisha mazingira ya kila Wilaya ili wananchi waendelee
kunufaika na miradi itakayoletwa na serikali ya Mkoa.
Comments
Post a Comment