Kukamilika
kwa ujenzi wa Zahanati ya Lukobe iliyopo Kata ya Kahama wilayani Ilemela,
kunatarajia kuleta ahueni ya upatikanaji wa huduma za afya kwa wakazi wa Mtaa
wa Lukobe ambao wamekuwa wakitembea umbali mrefu hadi kilomita 10 kusaka huduma
za afya.
Mradi huo
uliofunguliwa na Kiongozi wa mbio za Mwenge kitaifa jumapili Mei 19, 2019 ni
miongoni mwa miradi 10 iliyopitwa na Mwenge wilayani Ilemela ambapo ujenzi wake
ulianza baada ya kuibuliwa na wakazi wa Mtaa wa Lukobe na kuungwa mkono na Halmashauri
ya Manispaa ya Ilemela pamoja na mfadhili kutoka nchini Canada, Dawn Shaller.
Comments
Post a Comment