Uteuzi uliofanywa na Rais Magufuli leo akiwa Mbeya


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli amemteua Dkt. Moses Mpogole Kusiluka kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Taifa ya Uongozi ya Mfuko wa Maendeleo ya Jamii Tanzania (TASAF).

Dkt. Kusiluka ni Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Ikulu.
Wajumbe wa Kamati ya Taifa ya Uongozi ya TASAF ni;
  1. Balozi Zuhura Bundala
  2. Dkt. Dorothy O. Gwajima
  3. Dkt. Charles A. Mwamwaja
  4. Dkt. Ruth Rugwisha
  5. Dkt. Naftali B. Ng’ondi
  6. Mhandisi Hussein R. Mativila
  7. Bw. Richard Z. Shilambo
Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi imeeleza kuwa uteuzi huu umeanza tarehe 23 Aprili, 2019.

Comments