
Rais John Magufuli amesema muda wake wa uongozi ukiisha ataondoka madarakani tarehe hiyohiyo kwa kuwa yeye sio rais wa maisha.
“Mimi sio rais wa maisha ni rais wa
muda, nataka niwahakikishie muda ukimalizika nitaondoka tarehe hiyohiyo
ila kabla sijaondoka, maendeleo myapate kweli ili mwingine atakayekuja
aje ayaharibu mwenyewe na itakuwa dhambi yake kwa Mwenyezi Mungu,”
alisema jana alipokuwa akizungumza na wananchi wa Newala akiwa katika siku ya pili ya ziara yake mkoani Mtwara.
“Kwa hiyo nitasimamia (nchi) kwa
uadilifu mkubwa. Mafisadi wote nitalala nao mbele kwa sababu kutumbua
ndio nimeanza, ukila hela ya serikali hata kama una cheo gani utaondoka
tu.”
Alisema katika kipindi chake cha uongozi
maendeleo yameanza kupatikana ikiwamo ununuzi wa ndege, elimu bila
malipo, umeme maji na mambo mengine.
“Kwa hiyo mmenichagua nisimamie,
usimamizi ni kazi kubwa ndugu zangu, naomba tushikamane. Ninataka
Tanzania iwe ya viwanda,” alisisitiza.
Aliwataka viongozi wa Mkoa wa Mtwara
kusimamia viwanda vinavyoanzishwa bila kuchelewesha na kuonya asije
kutokea mfanyakazi yeyote wa kuzembe katika hilo.
Comments
Post a Comment