DC Nkumba akabidhi rasmi vifaa tiba

Mkuu wa Wilaya ya Bukombe Mhe. Said Nkumba tarehe 15 Machi, 2019 amekabidhi rasmi vifaa tiba vyenye thamani ya Tsh.  Million 20,540,000/= vilivyotolewa na Mhe. Doto Biteko Mbunge wa Jimbo la Bukombe wakati wa uzinduzi wa Zahanati ya Msasani iliyopo kata ya Bugelenga.

Nkumba alisema “vifaa tiba ambavyo vimetolewa na Mhe. Biteko navikabidhi rasmi kwenye Zahanati hii ili viweze kuwapunguzia hadha wananchi wa kijiji cha Msasani hasa akinamama wajawazito na watoto chini ya umri wa miaka mitano waliokuwa wanalazimika kwenda kijiji cha Bugelenga kwa ajili ya kupatiwa huduma za afya”.

Aidha  Nkumba ametoa wito kwa Diwani wa kata ya Bugelenda Mhe. Baraka Hussain kuhakikisha anakilea kituo hicho. ”Mh. Baraka hakikisha unakilea kituo hiki na usisubiri kuitwa, hakikisha unakuja kila wakati kuangalia zoezi zima  la utoaji wa huduma  linavyoendelea.”

Pia amewataka wanachi wa kata ya Bugelenga kuhakikisha wanashiriki shughuli za maendeleo kikamilifu ili waweze kupata fedha  za serikali zitakazosaidia katika ukamilishaji wa majengo yao kwani bila kufanya hivyo hakuna fedha yoyote ya serikali itakayotolewa bila ya uwepo ya nguvu zozote za wananchi.

Naye Mhe. Baraka amemshukuru Mhe. Biteko, uongozi wa Halmashauri pamoja na wananchi kwa kuhakikisha Zahanati hiyo inaanza kutumika kama ilivyokusudiwa.

Mganga Mkuu wa Wilaya Dr. Olden Ngassa amesema vifaa tiba vilivyopokelewa ni vitanda sita, magodoro sita, viti vya magurudumu (Wheelchair) 36 na stendi 15 kwa ajili ya mazoezi kwa wagonjwa wanye matatizo ya miguu

Comments