Waziri wa Madini, Doto Biteko akizungumza kwenye mkutano wa hadhara wa
Makamu Rais wa Tanzania, Mama Samia Suluhu Hassan uliofanyika hii leo
kwenye uwanja wa Kolimba, Wilaya ya Kaliua mkoani Tabora.
Mama Samia anaendelea na ziara yake ya siku tano mkoani Tabora iliyoanza
Februari 21, 2019 ambapo leo akiwa wilayani Kaliua, amekagua na kuweka
jiwe la ufunguzi kwenye jengo la upasuaji katika Kituo cha Afya Kaliua,
kukagua na kuweka jiwe la msingi ujenzi wa jengo la mama na mtoto katika
Hospitali ya Wilaya Kaliua. Pia amekagua na kuweka jiwe la msingi
kwenye ujenzi wa Kituo cha Afya Uyumbu kilichopo wilayani Urambo na
baadaye kuzungumza na wananchi kupitia mkutano wa hadhara.
Comments
Post a Comment