Makamu wa
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Samia Suluhu Hassan akizungumza
na wananchi kupitia mkutano wa hadhara uliofanyika katika wilaya ya Sikonge
mkoani Tabora.
Mama Samia
anaendelea na ziara yake ya siku tano mkoani Tabora aliyoianza Februari 21,
2019 ambapo hii leo amekagua na kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa ofisi za
Halmashauri ya Sikonge pamoja na kuzungumza na wananchi kupitia mkutano wa
hadhara uliofanyika katika uwanja wa TASAF.
Mkuu wa Mkoa Tabora, Aggrey Mwanri akizungumza jambo kwenye mkutano huo.
Jengo la ofisi za Halmashauri ya Wilaya Sikonge mkoani Tabora
lililowekewa jiwe la ujenzi na Makamu wa Rais, Mama Samia Suluhu Hassan.
Comments
Post a Comment