MAKAMU WA RAISI AKIWA KWENYE ZIARA MKOANI TABORA

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Samia Suluhu Hassan akizungumza na wananchi kupitia mkutano wa hadhara uliofanyika katika wilaya ya Sikonge mkoani Tabora.

Mama Samia anaendelea na ziara yake ya siku tano mkoani Tabora aliyoianza Februari 21, 2019 ambapo hii leo amekagua na kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa ofisi za Halmashauri ya Sikonge pamoja na kuzungumza na wananchi kupitia mkutano wa hadhara uliofanyika katika uwanja wa TASAF.
Mkuu wa Mkoa Tabora, Aggrey Mwanri akizungumza jambo kwenye mkutano huo.
Jengo la ofisi za Halmashauri ya Wilaya Sikonge mkoani Tabora lililowekewa jiwe la ujenzi na Makamu wa Rais, Mama Samia Suluhu Hassan.

Comments