CCM-GEITA YAWATAKA VIONGOZI KUWEKA MASLAHI YA TAIFA MBELE






Viongozi wa chama na serikali watakiwa kuweka maslahi ya Taifa mbele kwa kuacha ubinafsi ili kutengeneza nchi bora isiyo na mafisadi pamoja na wala rushwa 

Wito huo umetolewa na mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Geita Alhaj Said Kalidushi wakati akizungumza na Wanaccm Kata ya Igulwa Wilaya ya Bukombe Mkoani Geita iliwa ni mwendelezo wa ziara yake kwenye kata zote 17 za Wilaya hiyo. 

Kalidushi alisema viongozi wengi hawapendi kufanya kazi kwa hiari yao wanapenda kusumwa na kuwasihi kuiga mfano kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Taifa Dkt John Pombe Magufuli jinsi anavyojitoa kwa dhati juu ya Nchi katika kuhakikisha inaendelea kukua kiuchumi na kuzidi hakikisha amani yetu haipotei.

Aliwataka Wanaccm wa Wilaya Bukombe na Geita kwa ujumla kuwa waadilifu kwa kumchagua kiongozi bila kutumia rushwa na hatimae kupata kiongozi asiyekuwa na uwezo mzuri wa kuwahudumia wananchi na kuachana na makundi baada ya uchaguzi ili kulinda heshima ya Chama Cha Mapinduzi.


Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Wilaya ya Bukombe Daniel Machongo aliwataka Viongozi kujijengea uwezo mkubwa wa kusikiliza kero za wananchi na kuzitatua kwa wakati ili kuondoa lawama zisizokuwa za lazima

Pia Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Wilaya ya Bukombe Ladislous Soku aliwasihi viongozi wa chama na serikali kufanya kazi za wananchi bila ubaguzi ili kurahisisha utekelezaji wa ilani ya Chama Cha Mapinduzi kwa haraka.
 

Comments