“WAZAZI NA WALEZI ONENI UMUHIMU WA ELIMU KWA WATOTO ” DC NKUMBA


Mkuu wa Wilaya ya Bukombe Said Nkumba (pichani)


Wazazi na walezi Wilayani Bukombe Mkoani Geita, wametakiwa kupeleka wanafunzi waliofauru kujiunga na masomo ya sekondari mwaka 2019 kabla ya serikali kuwachukulia hatua za kisheria.

Wito huo umetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Bukombe Said Nkumba Ofisini kwake kutokana na kuwepo na baadhi ya wazazi na walezi kutopeleka wanafunzi kwa wakati na kusababisha wanafunzi wengi kutoroka nyumbani na kujiingiza kwenye vishawishi vya kuolewa, kufanya biashara ndogo ndogo na uchimbaji wa madini.

“Hakuna kitu kinachokera kama wazazi wasiopenda kusomesha watoto wao wakati serikali inatoa elimu bure
Wazazi wekezeni kwenye Elimu ili kutoa urithi wa kweli kwa watoto.”  Nkumba alisema.

Alisema amefanya ziara shule za sekondari na kukuta mwitikio wa wazazi wa kupeleka wanafunzi shuleni ni mdogo hadi alipo anza kuhamasisha viongozi wa vijiji na kata kuwashughulikia wazazi hali ambayo inaleta matumaini hadi sasa.

Nkumba alisema serikali haiwezi kukubali ikiwa mikakati ya serikali ya Wilaya ni kuanzisha kampeni ya kuhamasisha wazazi kusomesha watoto na kuchukuliwa hatua kali kwa  watakao kuwa hawaja wapeleka watoto shuleni.

Nkumba alisema shule za sekondari Wilayani hapa ni 15 lakini hadi Januari 16 mwaka huu inaonyesha takwimu ya wanafunzi walioripoti ni 3129  na 1325 hawajaripoti  kati ya wanafunzi waliofaulu 4467 mwaka 2018.
Amewataka wananchi kuiunga mkono serikali ya awamu ya tano  kwa wazazi kuhakikisha wanatumia frusa ya Elimu bure kuanzia chekechea hadi kidato cha nne kusomesha watoto wao kwa kuwanunulia vifaa na sale za shule.

 Ofisa mtendaji wa kata ya Butinzya Pamba Mgabali alisema kwamba wananchi bado wanamwamko mdogo wa kusomesha na kwamba kamati ya maendeleo ya kata  imekuwa ikihamasisha wazazi kupeleka wanafunzi shule na kuchangia mali zao kuboresha miundombinu ya shule.
Kwa upande wake Mkuu wa Shule ya sekondari Butinzya Sayi Gibe alianza kwa kumshukuru Mkuu wa Wilaya ya Bukombe Said Nkumba kwa kuchukua hatua za haraka kuanza ziara vijijni kwenda anahamasisha wazazi na walezi kuwapeleka watoto wao shuleni hali ambayo imeleta matokeo makubwa ya kuripoti wanafunzi kwa wingi.
Mwanafunzi wa kidato cha kwanza Butinzya sekondari  Saieda Gusho alisema wanafunzi wengi wanachelewa kutokana na wazazi wao kutowaanda watoto wao mapema kuwanunulia vifaa vya shule hali ambayo inawafanya kupitwa na masomo ya awali.




Comments