WANANCHI WA USHIROMBO WAPOKEA TATHIMINI YA MAENDELEO YALIYOFANYWA KWA MIAKA MITATU


Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Bukombe Daniel Machongo akipokea silaha za jadi kutoka kwa wazee wa Kata ya Ushirombo.


 Zahanati ya Kijiji cha Ihulike katika muonekano wa hatua iliyofikiwa baada Mhe. Doto Biteko(Mb)  kutoa mifuko 38 ya saruji ikiwa iliyotumika  hadi sasa ni mifuko ya saruji  20 na kazi bado inaendelea


Katibu wa Umoja wa Wanawake wa CCM Wilaya ya Bukombe akizungumza na wakazi wa Ushirombo.

Huyu ni mmoja wa wenyeviti wa wakitongoji kupitia Chadema akikapidhi kadi ya chama hicho na kujiunga na Chama Cha Mapinduzi 

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Bukombe Daniel Machongo akipokea Mwanachama mpya kutoka Chadema


Mkuu wa Wilaya ya Bukombe Said Nkumba akizungumza na wakazi wa Ushirombo.



     Wananchi wa Kata ya Ushirombo Wilaya ya Bukombe Mkoani Geita, wamepokea tathimini ya maendeleo ya kuanzia 2016 hadi 2018 iliyosomwa na Diwani wa Kata hiyo Lameck Warangi. 


Akitoa tathimini hiyo Warangi alianza kwa kuishukuru serikali na wadau wote wa Maendeleo kwa kuwashika mkono katika kuhakikisha Kata hiyo inaendeleo kupata maendeo na kubainisha upande wa elimu kwa mafanikio makuwa wanayoyapata kwa upande wa Sekondari ya Businda baada ya kuwa na maono ya kuwa na kidato tano na sita katika shule hiyo.


 Warangi alisema  wanataraji ndani mwaka 2019 zahanati ya Businda,Ihulike,Mwalo na Kiziba  zitakuwa zimeanza kutoa huduma kwa wananchi ili kupunguza adha ya kutembea umbali mrefu kutafuta huduma ya afya. 

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Bukombe said Nkumba alimshukuru sana Mbunge wa Jimbo la Bukombe kwa namna ya pekee anavyojitoa katika miradi ya maendeleo inayoendelea sehemu mbalimbali kwa Wilaya nzima na kuwaomba wananchi wa Kijiji cha Ihulike kuongeza bidii zaidi ili kuunga mkono jitihada za Mbunge wao baada ya kuwa ametoa mifuko 38 ya saruji kwa ajili ya ujenzi wa zahanati ya kijiji hicho.


 Pia aliwasisitiza wakazi wa Ushirombo na Wilaya nzima ya Bukombe kuhakikisha wazazi na walezi wanawaandikisha watoto wao shule ili kumuunga mkono Raisi wa Jamhuri ya Muungano Dkt John Pombe Magufuli kwa kutoa elimu bure sambamba na kusimamia kwa kushirikiana na walimu ili kujua maendeleo ya watoto hao na kutengeneza taifa la kesho lenye wasomi wengi.


Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Bukombe Daniel Machongo aliwapongeza wakazi wa Ushirombo kwa kujitoa katika shughuli za maendeleo bila kujali itikadi za vyama,dini wala ukabira na kuwakaribisha viongozi waliohamia CCM kwa hiari yao kutoka chama pinzani cha Chadema ikiwa katika uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka 2014 CCM walipoteza vitongoji vinane kwa Kata ya Ushirombo na tayari wamesharudi wenyeviti wanne na wengine wakiwa mbioni kujiunga na CCM.  

Comments