Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi John Kijazi, akimkabidhi Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Anna Mgwhira vitambulisho
wafanyabiashara wadogowadogo leo Jumatatu, Januari 28, 2019, Ikulu Jijini Dar es salaam.
Jumla ya vitambulisho milioni moja na laki moja vimekabidhiwa kwa wakuu
hao wa mikoa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi, ambavyo
viliasisiwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe
Magufuli mwishoni mwa mwaka uliopita.
Balozi Kijazi amekabidhi vitambulisho hivyo na kuwataka wakuu wa mikoa
hiyo kuhakikisha vitambulisho hivyo vinatolewa kwa wahusika na kwa
wakati kwa wahusika na kuongeza kuwa tayari kuna taarifa za baadhi ya
watumishi wa halmashauri ambao wanaviuza vitambulisho hivyo kwa zaidi ya
bei elekezi iliyotolea na Rais.
Pia amewataka wakuu hao wa mikoa kuwachukulia hatua za kinidhamu wale wote wanaokiuka agizo hilo.
Amewataka wakuu hao wa mikoa kusimamia kikamilifu zoezi hilo la ugawaji
wa vitambulisho kwa wafanyabiashara wadogo wadogo huku akitaja idadi ya
vitambulisho ambavyo kila mkoa utakabidhiwa.
Comments
Post a Comment