WAFANYABIASHARA WA SOKO LA KILIMAHEWA WAMSHUKURU MHE BITEKO






 Waziri wa Madini na Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe. Doto Mashaka Biteko akiwa na baadhi ya wafanyabiashara wakiangalia hatua iliyofikiwa katika ujenzi wa choo cha soko la Kilimahewa(picha ni ya zamani).


 Wafanyabiashara wa soko la Kilimahewa wakiwa katika umakini wa kumsikiliza Mhe. Doto Mashaka Biteko(Mb) 



 Tayari kwa Matumizi

Wafanyabiashara ndogo ndogo wa soko la Kilimahewa lililopo  Mji
 wa Ushirombo Wilayani Bukombe  wamemshukuru Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mkoani Geita Mhe Doto Mashaka Biteko baada ya kuwashika mkono katika ujenzi wa choo cha soko hilo.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti  sokoni hapo na Katibu wa soko la wajasiliamali Kilimahewa Gaudesia Nzumbi alisema soko liliazishwa mwaka 2001 na hadi sasa linameza 98 zinazofanyakazi na 80 wako nje ya soko pia kuna wenye maduka na wafanyabiashara wa nguo wanao uzia chini.

Nzumbi alisema  kabla ya kujenga choo wafanyabiashara walikuwa wanajisaidia kwenye nyumba za majirani na soko hilo na wengine vichakani hali ambayo ilikuwa changamoto kubwa kwa wafanyabiashara hao.

Mkazi wa Kilimahewa Janeti Paul  alisema wanaishukuru serikali na viongozi wengine waliohamasisha au kushiriki katika ujenzi wa choo cha soko ili kulinda Afya za wananchi wanaozunguka soko na wafanyabiashara wenyewe.

Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Katente Bahati Kayagila aliwaomba wafanyabiashara hao kuendelea kuibua miradi ya maendeleo na kuchangia maendeleo kila wanapo kubaliana kuanzisha mradi ili kupunguza au kuondoa changamoto zinazo wakabili na serikali itawashika mkono.

Waziri wa Madini na Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe. Doto Mashaka Biteko aliwachangia Tsh milioni  1.7 baada ya kuwatembelea na kujionea hali halisi ya wafanyabiashara hao na kuona nia yao baada ya kuchangishana wao kwa wao Tsh 4,000 kila mfanyabiashara kwa ajili ya ujenzi wa choo cha kisasa ili waondokane na changamoto ya muda mrefu ya kujisaidia sehemu zisizokuwa sahihi.

Comments