NMB YAKABIDHI MABATI 185 NA COMPYUTA SABA


 
 Jengo la Shule ya Sekondari Ushirombo  linalotarajiwa kuezekwa

 
Makabidhiano ya Mabati 

Makabidhiano ya Compyuta.


Benki ya NMB Tawi la Bukombe lakabidhi mabati 185 katika shule ya Sekondari Ushirombo na Compyuta saba kwa shule ya Sekondari Katente zilizoko Wilaya ya Bukombe Mkoani Geita. 


Wakati akikabidhi vifaa hivyo  Meneja wa Benki ya NMB Tawi la Kahama Richard Kirengo kwa niaba ya Meneja wa NMB Kanda ya Magharibi alisema changamoto za sekta ya Elimu Tanzania kwa Benki ya NMB ni jambo la kipaumbele,kutokana na ukweli kwamba Elimu ni muhimu kwa maendeleo ya Taifa lolote hapa duniani.

 
“Tunatambua serikali inafanya makubwa katika utoaji wa Elimu Bure na sisi kama wadau wa maendeleo tunawajibu wa kuunga mkono juhudi hizi  kwa kuisaidia jamii”. Kirengo alisema

 
Nae Meneja wa Benki ya NMB Tawi la Bukombe George Fundi alishukuru halmashauri na serikali ya wilaya ambavyo imekuwa ikitowa ushirikiano NMB na kwamba wataendelea kushiriki katika miradi ya maendeleo.

Mkuu wa Shule ya Ushirombo Sekondari Juma Luguhwa wakati akisoma taarifa yake wakati wa kukabidhiwa msaada wa mabati 185 yenye thamani ya Tsh milioni  5  yaliyotolewa  na Benki ya NMB Tawi la Bukombe yatakayo ezeka madarasa matatu ofisi moja ya walimu na  baada ya kupata mabati hayo  inaitajika Tsh milioni 39.74 ili kukamilisha  majengo hayo.



Kwa Upande wake Diwani wa Kata ya Bulangwa Yusuph Mohamed amewaomba wananchi kuchangia miradi ya maendeleo kwa hiari yao wanapoibua miradi na kuacha kuisubiri serikali iwafanyie kila kitu.                                          


 
Mkuu wa Wilaya ya Bukombe Said Nkumba alitoa shukrani kwa Benki ya NMB kwa kuunga mkono jitihada za serikali na kutoa wito kwa wadau wengine wa maendeleo kuendelea kutoa mali zao kwenye miradi ya maendeleo inayotekelezwa kwa nguvu za wananchi na serikali.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe Dionis Myinga alisema atahakikisha maelekezo ya Mkuu wa Wilaya yanafanyiwa kazi na kwamba wadau wa maendeleo waendelee kuchangia miradi ya maendeleo.




Comments