MIAKA MITATU YA MHE BITEKO JIMBONI



Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mkoani Geita, Doto Mashaka Biteko azungumzia miaka mitatu ya mafanikio katika miradi ya maendeleo kwa kushirikiana na wananchi na serikali.
Tangu  Mwalimu wa shule ya msingi Nyahanga hadi kuwa Afisa Elimu Taaluma Wilaya ya Nyag’hwale na  wadhifa wa umwenyekiti wa baraza la wazazi CCM Mkoa wa Geita, hatimae 2015 kuchaguliwa kuwa Mbunge wa Jimbo la Bukombe na kuteuliwa na Rais Dkt. John Magufuli kuwa Naibu Waziri wa Madini 2018 hadi Januari  8 mwaka 2019 kuteuliwa kuwa Waziri Madini na kuapishwa Januari 9 alipewa dhamana ya kuendesha Wizara ya Madini kitu ambacho kilikuwa ni kiu ya muda mrefu kwa wanabukombe kupata Waziri tangu Wilaya kuazishwa mwaka 1995.

Katika muonekano wa kawaida Mbunge wa Jimbo la Bukombe Doto Biteko anaonekana anashirikiana na wananchi, viongozi wa serikali na chama chake vizuri.
 Tangu achanguliwe kuwa Mbunge Oktoba 25 mwaka 2015 amekua akijishugulisha na wananchi kupitia mikutano ya hadhara na wengine kutumia njia nyingine kufanikisha maendeleo.
Kwa miaka mitatu aliyoiyafanya katika kuchagia maendeleo katika miradi iliyokuwa inaibuliwa na wananchi katika  vitongoji 373 vijiji 52 kata 17 tarafa 3.
Biteko amesema feha za kuchochea shughuli za maendeleo kwa kipindi cha mwaka 2015 hadi 2018 ametoa sh 102,037,797 zimetumika kutatua kero za wananchi hasa sekta ya Elimu, Afya na Maji, na vikundi vya wajasiliamali na kuchangia ujenzi wa vituo vidogo  vitatu vya polisi.

Amesema Jimbo la Bukombe linaukubwa wa kilometa za mraba zipatazo 8,055.59 kati yahizo kilometa za mraba 1766.59 ambazo sawa na asilimia 21.93 eneo la makazi na eneo linalo baki kilomita 6289 ni eneo la hifadhi za TFS na pori la hakiba Kigosi Muyowos huku jimbo lina watu 224,542 kutokana na sensa ya watu na makazi ya mwaka 2012.
Biteko amesema kutokana na ziara ambazo amekuwa akizifanya katika kipindi cha mwaka 2015 hadi Desemba 2018 ameulizwa na wananchi maswali 2567 ambayo yameulizwa kata zote 17 kutokana na kero mbali mbali zilizokuwa kwenye huduma za kijamii.

Kero hizo nilizikabiri kwa kushirikiana na madiwani na watalamu wa halmashauri na wadau wa maendeleo zipo changamoto ambazo zimetatuliwa kwa haraka na nyingine ninaendelea kuzitatua awamu kwa awamu na mabadiliko yanaonekana.
 
Amesema wakati anachaguliwa 2015 kulikuwa na zahanati nne vituo vya Afya viwili, lakini kwa sasa Jimbo la Bukombe lina zahanati 10 vituo vya Afya vinne na kwa kipindi cha mwaka 2018 katika kuhakikisha serikali inasongeza huduma kwa wananchi tumepata fedha kwa ajili ya upanuzi wa kituo cha Afya Uyovu  na Ushirombo.

Mwaka 2015 kulikuwa na mtandao wa barabara kilomita 256, lakini mpaka 2018 mtandao wa barabara umeongezeka kufikia  zaidi ya kilomita 1500 na kuwa Wilaya ya pili kimkoa kuwa na mtandao mkubwa wa barabara.
Amesema kuwa kutokana na serikali kuongeza bajeti ya wakala wa usambazaji wa umeme vijiji (REA) nimeendelea kufuatilia na kuhakikisha umeme  unasabazwa  vijiji vyote vya Wilaya ya Bukombe ili kufikia malengo ya kuifanya Bukombe nzima ipate Umeme na nguzo zinaendelea kusambazwa na mkandarasi.Biteko amesema.

Mkazi wa kijiji cha Uyovu Ester Maganga amsema kuwa maendeleo ya tofauti wameyaona tofauti na miaka mingine  wamekuwa wakiona maendeleo bila kuchangishwa wananchi ikiwemo shule ya watoto wenye mahitaji malumu iliyopo shule ya msingi Uyovu na Ushirombo.

Maganga ameongeza kuwa Mbunge ni wakati wa kujitathimini kupitia aliyoyafanya kwa miaka mitatu na kwamba asije akachoka kuwaletea maendeleo wana Bukombe ili uchanguzi mkuu 2020 atumie dakika 45 na za nyogeza 3 ili kuwa na historia  ya kwenda Bungeni awamu mbili na huenda Rais Magufuli ataendelea kumuacha na nafasi yake. 

 Katibu mkuu wa CCM Taifa Bashiru Ally amesema  wakati wa ziara yake Wilaya ya Bukombe wakati Mbunge Biteko anawasilisha taarifa ya utekelezaji wa Ilani  ya CCM kwa aliyoyafanya kwa miaka mitatu alimpongeza.

Ally aliwahimiza wabunge na viongozi wa chama na serikali kusimamia sekta ya kilimo ikiwa ni nguzo inayotegemewa na taifa kwa kuinua uchumi  kwa wananchi wake hivyo wasaidizi wa Rais Dk John Magufuli kuanzia ngazi ya Wilaya na Mkoa kushuka chini wahakikishe wanaelimisha wakulima namna ya matumzi ya mbegu bora

Ally aliwataka Wakuu wa Wilaya na Mkoa kuhamasisha wakulima kulima na kupanda mbegu bora na kufunga mifungo kwa kuzingatia ufungaji wa kitalamu ili kupata maligafi kwenye viwanda wakati Tanzania ikielekea kwenye uchumi wakati na viwanda.

 Mkuu wa Wilaya ya Bukombe Said Nkumba amewaomba wananchi wilayani hapa kuunga mkono jitihada za wadau wa maendelo ili kufikia malengo ya miradi walio ianzisha.

Nkumba amesema Mbunge kwa namna ya pekee anavyojitoa katika miradi ya maendeleo inayoendelea sehemu mbalimbali wilayani hapa sekta ya Elim na Afya wananchi na wadau wa maendeleo inawapasa kumuunga mukono.

Comments