
Ladislaus alisema mpango wa Halmashauri ni kuhakikisha vituo vyote vya kutolea huduma za afya vinaanzisha madarasa lishe kwa ajili ya kupunguza changamoto inayowakabili watoto chini ya umri wa miaka 5 kwa kuwa mpaka sasa jumla ya watoto 227 katika kata ya Bugelenga waliopimwa uzito kati yao watoto 113 wanalishe bora na watoto 114 wanautapiamlo (unauzito pungufu kulingana na umri wao).
Pia amewaomba mafisa elimu Msingi na Sekondari kuhakikisha wanawasisitiza wakuu wa shule pamoja na walimu wakuu kuanzisha mpango wa chakula shuleni ili wanafunzi waweze kupata chakula bora wakiwa shuleni.
Akichangia taarifa ya kampeni ya utoji wa vitamin A katika kikao hicho Mratibu wa chanjo Wilaya Ndg Simon Misusi alisema kupitia mpango wa kumfikia kila mtoto kwa chanjo wameweza kuhamasisha vituo kumi ambavyo ni hospitali ya Wilaya ya Bukombe, kitu cha Afya Uyovu, Ikuzi, Ushirombo, Iyogelo, Bugelenga, Mienze, Bukombe pamoja na Bugando na kuhakikisha watoto wote kuanzia miezi 6 hadi miezi 59 wanapata vidonge vya vitamin A pamoja na dawa za minyoo.
Akihitimisha kikao hicho Mkuu wa Idara ya Kilimo Ndg. Joseph Machibya kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji aliwaomba wajumbe kuhakikisha wanaweka shughuli za lishe kwenye bajeti ya mwaka wa fedha 2019/2020 ili kupata watoto wenye afya njema ambao watakuwa viongozi kwa siku za baadaye.
Comments
Post a Comment