SERIKALI YAUKATAA MPANGO WA UFUNGAJI MGODI WA BUZWAGI





Serikali imeitaka kampuni ya Acacia kuandaa na kuwasilisha haraka mpango mpya wa urejeshaji mazingira katika hali yake ya kawaida baada ya kusitisha shughuli za uchimbaji dhahabu katika mgodi wa Buzwagi uliopo wilayani Kahama ifikapo mwaka 2020.


Naibu Waziri wa Madini, Doto Biteko aliyasema hayo jana alipofanya ziara katika mgodi huo kukagua shughuli zinazoendelea mgodi hapo.


Mapema mwaka huu, Wizara ya Madini iliukataa mpango uliokuwa umeandaliwa na kampuni hiyo ukikadiriwa kutumia dola milioni 18 kwa kuwa haukujumuisha kufukiwa baadhi ya mashimo mgodini hapo (tazama picha), bali yabaki wazi hadi yatakapojaa maji katika kipindi cha miaka 100 ijayo. 





Naibu Waziri Doto Biteko (katikati), akifafanua jambo wakati akikagua shughuli mbalimbali katika mgodi wa Buzwagi.
Naibu Waziri Doto Biteko akielekea kukagua sehemu ambapo mchanga wenye madini (makinikia) umehifadhiwa ndani ya mgodi wa Buzwagi.
Tazama Video hapa chini 

Comments