WALIMU WA MICHEZO WAHIMIZWA KULETA USHINDI UMITASHUMITA








Afisa Tawala Wilaya ya Bukombe Mkoani Geita, Ally Mketo amewahiza walimu wa shule mbalimbali za msingi Wilayani hapa wanaowasimamia wanafunzi wamichezo ya umitashumita wahakikishe wanashika namba moja kimukoa.
Mketo aliyasema hayo wakati wa uzinduzi wa michezo ya wanafunzi umitashumita katika viwanja vya shule ya Sekondari Ushirombo  wanafunzi hao wanafanya michezo kwa siku tano kisha wanaenda kukutana na timu zingine za michenzo mbali mbali.
Alisema walimu wa michezo wahakikishe ushindi kimukoa wanauleta Bukombe kwa kuzingatia misingi ya michezo  na miongozo mizuri kwa wanamichezo kwa kuzingatia nidham na upendo baina yao.
Kwa upande wake Afisa michezo  Wilaya ya Bukombe Jenipha Kisusi alisema kuwa michezo hiyo ya umitashumita umeshirikisha wanafunzi toka tarafa ya Siloka, Ushirombo, Bukombe na wanafunzi wanao shiriki  209 wavulana 126 wasichana  83  walimu wa michezo 21 wakiume 14 wakike 7.
Kisusi alisema wanafunzi hao wanashiriki michenzo ya mpira wa miguu, Pete, wavu, mikono,sanaa na riadhaza aliongeza kuwa ndani ya mafanikio hayo ya kuwapata wanafunzi wenye vipaji  wamekutana na changamoto za wazazi kutokuwa tayali kuluhusiu watoto wao kushiriki na wanakabiliwa na ufinyu wa bajeti  aliomba wadau wa michezo kuwachangia watoto hao ili wakafanye vizuri .
Kwa niaba ya Afisa Elimu Wilaya Sida Shalali alimuhakikishia mgeni rasimi Afisa tawala Wilaya Ally Mketo kuwa wanafunzi na walimu wamepewa maelekezo ya kuleta Umbingwa Bukombe aliwaomba wananchi wa wilaya ya Bukombe kuendelea kuwaombea watoto  mungu awasaidie wafanye vizuri walete ubigwa wa michezo ya umitashumita.

Comments