VIONGOZI WA MAZEHEBU YA DINI WAHIMIZWA KUKEMEA IMANI POTOFU


Viongozi wa madhehebu ya Dini Wilaya ya Bukombe Mkoani Geita, amewahimiza kufundisha waumini wao kuondokana na imani potofu za kuamini ushirikina na watu wenye ualbino kuwa ni dili badala yake washirikianae kupinga mauaji ya wazee kwa imani potofu na watu wenye ualbino kwa madai kuwa viungo vyao ni utajili.
Wito huo ulitolewa na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani Eng Hamad Masauni  ambae alikuwa Mgeni rasmi katika hafla ya kufuturisha waumini na viongozi wa dini ya waislamu Wilayani hapa iliyo hudhuliwa na viongozi wa vyama vya siasa na serikali kutoka sehemu mbalimbali nchini iliyokuwa imeandaliwa na Naibu Waziri wa Madini pia Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe. Doto Mashaka Biteko katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe.
Masauni aliwaomba waumini wa dini ya kiislamu na mazehebu mengine kuendeleza upendo kwa watu wote na waumini wa kiisilamu aliwasisitiza kudumu katika imani ya kiisilamu wakati wote na kusimamia mafundisho waliyoyapata wakati wa mwenzi mtukufu wa ramadhani.
 
Mjumbe wa Halmashauri kuu ya Taifa BAKWATA Shekh Hasan Kabeke alisema waisilamu wengi wamekuwa wakishika imani za dini wakati wa mfungo wa mwenzi mtukufu kisha kusahau kwa muda mfupi hali ambayo inamchukiza mwenyezi mungu.
 
Kabeke aliwataka waisilamu kuwa mfano bora katika jamii kwa kueshimu misingi ya kidini na sheria za nchi na kujikumbusha kunyeyekea na kudumu katika mafunzo ya kiisilamu. 

Naibu Waziri wa Madini ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe. Doto Mashaka Biteko aliwashukuru waislam kwa dua zao njema za kuiombea Wilaya ya Bukombe na Tanzania kwa ujumla ili iendelee kuwa kisiwa cha amani.
Biteko aliwahimiza waislamu na waumini wa madhehebu mengine  kuendelea na ushirikiano wa kuwaombea viongozi wa serikali ya awamu ya tano ili kila wanacho kifanya kiwe na kibali cha kimungu kwa masilahi ya taifa.

Biteko aliwaomba viongozi wa madhehebu ya dini kuhamasisha waumini kusomesha watoto na kufanya kazi za maendeleo kwa kuzingatia sheria na kuacha kuingiza siasa kwenye maendeleo badalayake waibuwe frusa za kiuchumi kwa kufanya ujasilimali hali ambayo itawafanya kuongeza pato la famiiia na taifa.















Comments