WATALAMU WA AFYA WAJENGEWA UWEZO MPYA WA KUNUNUA VIFAA TIBA



Watalamu wa idara ya afya,fedha,mipango na ICT kutoka katika halmashauri za  Mkoa wa Geita wamepokea mafunzo ya mfumo mpya wa ugatizi wa madaraka kwa kupeleka fedha moja kwa moja katika vituo vya kutolea huduma za afya,mfuko wa Bima ya afya iliyoboreshwa kwa jamii ICHF  pamoja na matumizi ya fedha na ununuzi wa dawa na vifaa tiba (JAZIA).

Akifungua mafunzo hayo ya siku tatu Wilayani Bukombe Katibu Tawala wa Mkoa wa Geita Selestini Gesimba alisema mafunzo hayo yatawaimarisha ili wafanye kazi kwa ufanisi na wepesi zaidi
 
 Gesimba alisema awali kulikuwa na changamoto kwa wananchama wa CHF    walikuwa  hawatibiwi nje ya Wilaya kabla ya kuboreshwa  lakini  kwa sasa kunamabadiliko makubwa yaliyofanywa na serikali mwanachama anatibiwa Wilaya yeyote hapa nchini na kuwaomba wanaoshiriki mafunzo hayo kuhakikisha wanawaelimisha wananchi ili wanufaike na huduma za afya zilizo boreshwa (ICHF).

Nae Mganga Mkuu wa Mkoa wa Geita Dk Japhet Simeo amekili kuwepo kwa baadhi ya changamoto ya ucheleweshwaji wa upatikanaji wa dawa na vifaa tiba kwa wakati na kwamba kupitia mfumo huu mpya kutarahisisha upatikanaji wa dawa kwa muda sahihi.

Kwa upande wake Mshauri wa Menejimenti ya dawa katika mradi huo Fiona Chilunda alisema Serikali Mkoani Geita kupitia mradi wa Tuimarishe Afya (HPSS) ulioanza kwa kutekelezwa kwenye mikoa mitatu na hatimae  nchi nzima  kwa kushirikiana na serikali ya Tanzania na Uswis  imekusudia kuendelea kupunguza changamoto  za upatikanaji wa dawa pamoja na vifaa tiba kuanzia  kwenye vituo vya afya, zahanati na hospitali zote nchini.

Kaimu Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bukombe Dk Irine Mkerebe   alipongeza serikali ya Tanzania kwa kuwa na ushirikianao na serikali ya Uswis hali ambayo italeta mabadiliko makubwa kutokana na mafunzo wanayopewa huku hoja hiyo ikiungwa mkono na  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Chato Dk Athanas Ngambakubi akisema kupitia mafunzo hayo kutasaidia kupunguza baadhi ya changamoto kwenye idara ya afya Mkoani hapa.

Comments