WALIMU WAOMBA SERIKALI IWAKUMBUKE WALIOSAHAULIKA KUPANDISHWA MADARAJA

Walimu wa shule ya msingi Kata ya Namonge Wilaya ya Bukombe Mkoani Geita, wameiomba serikali iwakumbuke walimu kuwapandisha madaraja walimu ambao wanasifa hiyo ikiwa ni haki yao kama watumishi.


Rai hiyo ilitolewa na mkuu wa shule ya msingi Namonge Jemes Kadogo wakati wa sherehe ya kwanza tangu 2002 shule hiyo kuazishwa, akisoma risara kwa mgeni rasmi huku akibainisha changamoto zinazawakabili walimu ikiwa ni pamoja na upugufu wa miundo mbinu ya shule na walimu 21 wakiwa na sifa za kupandishwa madaraja mbali mbali ya kitaluma lakini wamekuwa wakipigwa dana dana wanapo fuatilia suala hilo.
Kadogo  alimuomba Diwani wa Kata ya Namonge Mulalu Bundara ambae alikuwa ngeni rasmi kwenye sherehe za Mei Mosi iliyokuwa imeadaliwa na walimu wa shule hiyo  alisema.
“muwakilishi wa wananchi na watumishi wa umma  kata ya Namonge katika vikao vya baraza la madiwani halmashauri ya Bukombe tunaomba sana utusaidie ili ofisi ya Elimu iwape sitahiki zao za kimsingi walimu ikiwa shule iliazishwa 2002  mpaka sasa kuna walimu 25  wanafunzi 2859 wanasitahili kusomea kwenye vyumba vya madarasa 63 lakini wanasomea madaradasa 11 walimu wanaohitajika 62 waliopo 25 kati yao 21 wanamda mrefu hawajapandishwa madaraja”alisema Kadogo.

Muwakilishi wa CWT tawi la Namonge shule ya msingi Justina Malifedha aliwaomba walimu wezake kuwa na ushirikiano na  kufanyakazi kwa kuzingatia mipaka ya kufanyakazi kwa kujituma ili kuinua Elimu Wilaya ya Bukombe na Taifa kwa ujumla.

Diwani wa Kata ya Namonge Mulalu Bundara aliwaomba walimu kuwa maswala ya kupandishwa madaraja yanataratibu zake na kuwahakikishia kuwa atalifatilia kama mwakilishi wao na aliwakumbusha kuwa kazi ya uwalimu ni wito wahakikishe  wanaendelea kufanyakazi vizuri ikiwa shule hiyo imeingia kwenye 10 kati ya shule 78 za Wilaya kwa mika mitatu tangu mwaka 2015.
Bundara aliwaomba walimu kutambua fursa za kiuchumi na kuwekeza kwenye ujasiliamali wakati wakiwa na ajira serikalini ili watakapo fikia umri wa kustaafu wasianze kujifunza kazi za ujasiliamali badala yake waanze mapema kuzitambua fursa.

Bundara alikemea bazi ya walimu wamekuwa na tabia ya ulevi wa kupindukia kila unapofika mwisho wamwezi wanasahau na famila zao wakidai kuwa chezea mshahara usicheze  kazi huku wanajiadalia umasikini na kuishi maisha dunu tena magumu watakapo staafu wakati huu ndo wa kujipanga na maisha na kuwa mfano wa kuingwa najamii bada ya kustaafu.
 
Mratibu Elimu Kata ya Namonge Alex Nkingwa alisema madai ya walimu hao anayajuwa na kwamba yametolewa ufafanuzi na Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dk John Magufuli baada ya kuwasilishwa na vyama mbali mbali vya watumshi kwenye sherehe za kitaifa katika viwanja vya Samola Mkoani Iringa.

Comments