Mashindano ya michezo yanayoendeshwa na Taasisi ya The
Angeline Foundation yanayotarajiwa kuanza siku chache zijazo yatagawa
vifaa vya michezo kwa timu shiriki kutoka makundi mbalimbali yaliyopo
ndani ya Jimbo la Ilemela
Kauli hiyo imetolewa leo na mgeni rasmi wa fainali za
mashindano ya mpira wa miguu Mhe Bhiku Kotecha ambae ni Naibu Mstahiki
Meya wa Halmashauri ya Jiji la Mwanza yaliyoshirikisha Timu zaidi ya 14
huku Timu 9 zikiwa ni za matawi ya Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama
Cha Mapinduzi UVCCM na Timu 5 zikitoka makundi maalumu kama Vyuo Vikuu,
Waendesha Matoroli, Waendesha bodaboda na Jeshi la polisi yaliyojukikana
kama Ramadhani Cup ambapo akiwasilisha salamu za Mbunge wa Jimbo la
Ilemela Mhe Dkt Angeline Mabula amesema kuwa Mbunge wa Jimbo hilo
atagawa vifaa vya michezo kwa Timu zote zitakazoshiriki mashindano ya
Jimbo Cup pamoja na kusisitiza juu ya kukubali matokeo iwe kushindwa ama
kushindwa ili kuepusha vitendo vya uvunjifu wa amani
'... Waziri kaniagiza niwaambie yupo pamoja nanyi na katika
mashindano ya mwaka huu atagawa vifaa vya michezo na mipira kwa timu
zote zitakazoshiriki lakini mtambue tu katika michezo kuna kushinda na
kushindwa ni lazima tuwe teyari kwa lolote litakalojitokeza ...' Alisema
Aidha Mhe Kotecha ameziasa timu za Taasisi kuhakikisha
zinashiriki mashindano hayo sanjari na kuwataka vijana wa mkoa wa Mwanza
kuwa mstari wa mbele katika kutumia fursa mbalimbali za kujiletea
maendeleo zinazojitokeza.
Kwa upande wake Katibu wa UVCCM kata ya Kirumba Comrade
Amiri Biliyomo amefafanua juu ya malengo ya kuanzisha mashindano hayo ya
Ramadhan Cup ikiwa ni pamoja na kurudisha hamasa kwa vijana katika
kuungana pamoja, kujiepusha na vitendo viovu ikiwemo matumizi ya madawa
ya kulevya, wizi na vitendo vingine vya uvunjifu wa amani.
Mashindano ya Ramadhan Cup yalihudhuriwa na viongozi
mbalimbali wakiwemo UVCCM mkoa Mwanza walioongozwa na Mwenyekiti wa
Jumuiya hiyo, UWT walioongozwa na Katibu wa Jumuiya hiyo ngazi ya mkoa,
Viongozi wa Chama na Jumuiya zote za wilaya ya Ilemela ambapo yaliisha
kwa Timu ya Polisi Ilemela kuicharaza vikali Timu ya Kirumba Kati goli
moja kwa sifuri lililofungwa katika kipindi cha Pili dakika ya 35 na
mchezaji wao machachari Emmanuel Maba na kujifanya timu hiyo kuondoka na
mbuzi wawili pamoja na kombe.
' Ilemela ni yetu, tushirikiane kuijenga '
Imetolewa na
Ofisi ya mbunge
Jimbo la Ilemela
27.05.2018.
Ofisi ya mbunge
Jimbo la Ilemela
27.05.2018.
Comments
Post a Comment