SERIKALI KUTOA MASAA 72 KWA WAFANYABIASHARA WADOGO WADOGO WALIOJENGA VIBANDA CHINI YA NYAYA ZA UMEME WA TANESCO KUONDOA
Serikali Wilayani
Bukombe Mkoa wa Geita imetowa maasa 72 kwa wafanyabiashara wadogo wadogo
wa nafaka na matunda waliojenga vibanda chini ya nguzo za umeme wa TANESCO mtaa
wa Uhamiaji Kata ya Katente Wilayani hapa kuondoa ili kupisha miundombinu hiyo.
Rai hiyo ilitolewa na Mkuu wa Wilaya hiyo Josephat Maganga kwenye
mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya Butambala baada ya malalamiko ya uvunjwaji wa sheria yaliyofikishwa
kwenye kamati ya ulinzi na usalama na halmashauri kupita idara ya ardhi
pamoja na shirika la umeme Tanzania TANESCO na kamati ikafatilia na kujiridhisha kuwa
wananchi wamejenga vibanda chini ya Nguzo za umeme kwa madai kuwa wamepewa na Chama
Cha Mapinduzi CCM Wilaya ya Bukombe hali ambayo si kweli.
Maganga alishirikiana na watalam mbalimbali kutoa elimu kwa
wananchi wa Kata nne Katente,Ushirombo,Igulwa, Bulangwa, juu ya madhara ya umeme.
Alisema kutokana na kubaini kuwa kuna uvunjaji wa sheria
mkubwa uliofanywa na wafanyabiashara hao kwa kujenga vibanda chini ya nyaya za
umeme zenye Msongo Kilovoti 33 baada ya kugawiwa ki holela aliwasihi kuviondoa
kupisha miudo mbinu hiyo baada ya masaa 72.
Pia alimuagiza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
kuharakisha maeneo yaliyotengwa kwa ajili biashara ya soko yanalipwa fidia
mapema tayari kwa kuwagawia wananchi hao.
Meneja wa shirika la umeme Wilaya ya Bukombe Thadey Mapunda alisema mradi huu kwa awamu ya kwanza
vitongoji na vijiji 80 vinanufaika na
kwamba sheria zinataka njia ya umeme iwe wazi na asiwepo mwananchi wa kuvamia
kufanya shughuli yeyote ya kibinadamu chini ya nguzo za umeme ili kuepuka athari
inayoweza kujitokeza kuaguka nguzo ama waya.
Miongoni mwa wafanyabaishara waliojenga vibanda kwenye maeneo
hayo Adam Machungwa alitupia lawama serikali kwa
kuwaingiza mkenge wananchi wake kutumia ghalama kubwa kisha kuwafukuza hali
ambayo inaludisha maendeleo nyuma kwa wananchi wa maisha ya chini.
Machungwa alisema walipewa na viongozi wa serikali za mitaa Aprili
mwaka huu waliaza kujenga vibanda,lakini serikali hiyo hiyo inatufukuza wakati tumejenga kwa
ghalama za kuuza kuku za kufuga zikiwemo bidha mbali mbali za ndani.
Hoja hiyo iliungwa
mkono na barozi wa nyumba 10 mstafu mtaa
wa Bomani Suzana Giti alisema waligawiwa maeneo hayo kwa lengo la wananchi wafanye shughuli za
ujasiliamali ili kujikwamua na umasikini aliomba seriakli kutowanyang’anya maeneo
hayo badalayake waruhusiwe kuyaendeleza
kwa kufanyia biashara.
Comments
Post a Comment