Wanafunzi wa kidato cha nne 2016 Shule ya Sekondari Ushirombo wakipokea unga,maharage na mchele ikiwa ni motisha ya chakula kutoka kwa Mbunge wa Jimbo la Bukombe na Naibu Waziri wa Madini Mhe. Doto Mashaka Biteko ili wakae shuleni hapo kwa ajili ya maandalizi ya mtihani wa taifa (picha hii ni ya 2016)
Mwanafunzi aliyefanya vizuri kwenye mtihani wa kumaliza kidado cha nne mwaka 2017 shule ya Ushirombo sekondari Kata ya Bulangwa Wilaya ya Bukombe Mkoani Geita,Bonephace Bagasa amepokea motisha baada ya sh 100,000 na Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe. Doto Mashaka Biteko ikiwa ni moja ya ahadi zake kwa wanafunzi wa shule hiyo kwa watakao faulu.
Akizungumuza shuleni hapo baada
ya kukabidhiwa mbele ya wanafunzi wa shule hiyo Bagasa alimshukuru Mbunge kwa kujitoa kuhamasisha ufaulu kwa wanafunzi na kuomba viongozi wengine waige mfano huo.
Bagasa alitoa wito kwa
wanafunzi kuwa ili wafanye vizuri inawapasa kuheshimu wazazi na walimu na
kuachana na makundi lika wanapokuwa shuleni na nyumbani aliwasihi kujitengea
munda wa kujisomea wakiwa nyumbani na kujituma wakiwa shuleni.
Mkuu wa shule msaidizi Ushirombo Sekondari Mabula Ngela alisema mwaka 2017 wanafunzi watahiniwa walikuwa 266
wavulana walikuwa 162 wasichana 104 lakini mwanafunzi Boniphace Bagasa alifaulu
kwa kupata divisheni 1peke yake.
Ngela alimpongeza na kumshukru Mbunge wa Jimbo la Bukombe Doto Biteko kwa kutimiza ahadi yake aliyoitowaga shuleni
hapo wakati wa mahafali ya wanafunzi hao mwaka 2017 kuwa mwanafunzi atakaye
pata divisheni 1 atampa motisha hali ambayo iliawafanya wanafunzi kujituma
kwenye masomo.
Pia aliahidi kuongeza ufaulu ili kutomvumja
moyo Mbunge kwa kutoa mitihani ya majaribio ya mara kwa mara kwa wanafunzi 206
ambao wako kidato cha nne mwaka 2018 .
Alisema wamejiwekea mikakati ya
kudhibiti hali ya utoro ikiwa hali ya nyuma kulikuwa na utoro kwa kushirikiana
na wazazi na walezi na kwamba wamekuwa wakihamasisha wanafunzi kujisomea na
wazazi kuwatengea munda wakujisomea wanapokuwa nyumbani.
Katibu wa Mbunge wa Jimbo la Bukombe Benjamin Elias Mgeta akikabidhi motisha hiyo kwa niaba ya Mbunge wa Jimbo la Bukombe na Naibu Waziri wa Madini Mhe. Doto Mashaka Biteko aliwaomba wazazi na walezi kuwekeza kwenye elimu
ili kuwawezesha vijana kufanya shughuli za kujiajiri kwa ufanisi mzuri na wengine kuajiliwa na
serikali pamoja na sekta mbalimbali nchini.
Mgeta aliwaomba walimu
kutambua kazi yao ni ya wito hivyo wahahakikishe wanatimiza wajibu wao kwa kuzingatia
maadili ya utumishi na kuishi vizuri na jamii inayowazunguka.
Comments
Post a Comment