MBUNGE AKUTANA NA VIONGOZI WA CHAMA KATIKA KIKAO CHA KAZI.

Mbunge wa Jimbo la Bukombe na Naibu Waziri wa Madini Mhe Doto Mashaka Biteko amezungumza na Wenyeviti,Makatibu na Makatibu Wenezi wa Kata zote za Wilaya ya Bukombe kwenye kikao cha kazi kilichofanyika katika Ukumbi wa Chama Cha Mapinduzi Wilayani Bukombe.
 Akizungumza na Wajumbe hao alianza kwa kuwapongoza kwa kuchaguliwa kwao na kuwaomba wasimamie katika kuhakikisha wanamaliza makundi ndani ya chama yaliyojitokeza wakati wa uchaguzi kwa kuimarisha upendo na mshikamano baina yao sambamba na kuwaomba wazidi kuunga mkono Serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Mhe Dkt John Pombe Magufuli dhidi ya utetezi wake kwa wananchi wanyonge wenye kipato cha chini.
Pia aliwasisitiza viongozi hao wa chama kushirikiana na watumishi wa serikali katika kuhakikisha Ilani ya chama cha mapinduzi inatekelezwa kikamilifu huku akibainisha miradi iliyotekelezwa Wilayani humo ikiwa ni pamoja na kuongezeka kwa vituo vya Afya huku vilivyopo vikiboreshwa na kupanuliwa,Mradi wa umeme vijijini (REA) kusambaza vijiji vyote Wilayani humo,kutatua changamoto ya  maji kwa kuanzisha miradi midogo ya maji,ujenzi wa vyumba vya madarasa katika shule mabalimbali ikiwemo Ibamba na Namonge kwa shule za msingi,vyumba sita vya madarasa Ushirombo sekondari,  mitandao ya barabara kuongezwa hadi kilomita 1500 na kuwa ya pili kwa Mkoa wa Geita kwa kuwa na mtandao wa barabara nyingi.  
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi CCM (W)Bukombe Daniel Machongo aliwapongeza wajumbe kwa mahudhurio yao na kuwaomba wajitume kikamilifu kukijenga na kulinda chama hicho ili kiweze kuwa na serikali imara.



Comments