Watu 602 Kata ya Uyovu Wilaya ya Bukombe Mkoani
Geita, wamejitokeza kujua afya zao kwa kupima kwa hiyari VVU kati yao wanaume 413 wanawake 189
kati hao waliokutwa na maambukizi ya VVU ni 26 sawa na asilimia 12 ya maabukizi
ya UKIMWI ikiwa wanawake 12 wanaume 14.
Taarifa hiyo ilitolewa na Mkuu wa Wilaya ya Bukombe Josephat Maganga
wakati wa makabidhiano ya Mwenge wa Uhuru na wakimbiza mwenge 2018 kwa Mkuu wa Wilaya ya Chato Shaban Ntarambe katika viwanja vya Kijiji cha Nyarututu Kata
ya Bwanga Wilaya ya Chato.
Maganga alisema kutoka Uyovu hadi eneo la kukabidhi mwenge wa
uhuru ulikimbizwa kilomita 45 aliwapongeza wananchi kujitokeza kupima VVU na
kuchangia damu kwa hiyari kwenye mkesha wa mwenge wa uhuru Kata ya Uyovu wananchi
walichangia kwa hiyari chupa za damu 19.
Maganga alisema mwenge
wa uhuru Wilaya ya Bukombe umegharimu Sh Sh21,577.50 kutoka kwa wadau wa
maendeleo, wananchi, halmashauri ya Wilaya
na serikali kuu, fedha hizo zimefanikisha shughuli mbalimbali za mwenge
ikiwemo chakula,vinywaji, ujenzi,mapambo,Burudani, hamasa na usafiri.
Maganga akizungumuza
kwa niamba ya wananchi wa Wilaya ya Bukombe alisema mwenge wa uhuru ulikimbizwa kilomita
85 na kupitia miradi ya maendeleo 8
mmoja wa kuwekewa jiwe la msingi,
mwingine mmoja wa kufunguliwa, miradi miwili ya kuzindua, miradi mingine minne ya kuona na kufunguliwa
yenye thamani ya Sh1,154,811,623.40.
Alichanganua kuwa Nguvu za wananchi Sh 73.204 milioni
halmashauri sh 8.763 milioni wahisani sh316.740 milioni serikali kuu sh 810.77
milioni.
Kiongozi wa mbio za mwenge wa uhuru Charles Kabeho
aliwapongeza wananchi wa Wilaya ya Bukombe na viongozi wa serikali na
wamadhehebu ya dini na kuwataka kuendelea kuwekeza kwenye Elimu na kutambua afya
kwa kupima kwa hiyari na kama mtu amepatikana na maambukizi ya UKIMWI kwa
bahati mbaya atumie dawa za kufubaza virusi na akizingatia ushauri wa madaktari ili aendelee kufanya kazi zake vizuri zikiwemo za uzalishaji mali.
Comments
Post a Comment