WANAUME WILAYANI BUKOMBE WAASWA KUACHANA NA IMANI POTOFU YA MADAI KUWA VYANDARUA VINAMALIZA NGUVU ZA KIUME

Kiongozi wa mbio za mwenge wa uhuru mwaka 2018 Charles Kabeho ametoa wito kwa wanaume wanaozuia matumizi ya vyandarua katika familia zao kwa kuwa na mila potofu za madai kuwa wanapo lala kwenye chandarua wanakumbwa na tatizo la upungufu wa nguvu za kiume na kuzalisha wadudu aina ya  kunguni ndani.
Rai hiyo ameitoa wakati akizungumza na wananchi wa Kata ya Iyogelo Wilaya ya Bukombe Mkoani Geita Kabeho amewaomba wanaume kuachana na dhana potofu ambazo hazina ukweli wowote hali ambayo imekuwa ikiwasababishia familia nyingi kuugua maralia na kusababisha watu wasifanye kazi za kuingiza pato la familia na taifa kwa kwenda kutafuta huduma za afya kwa ajili ya matibabu.
”acheni mila potofu za madai kuwa mwanaume akilala kwenye kitanda chenye chandarua atapunguza nguvu za kiume si kweli niupotoshaji mkubwa wa jamii Mungu akiwa amekuumba na nguvu za kiume za kutosha hata kama ungelala kwenye chandarua hazitapunguwa hata kidogo tumieni chandarua safi na kusafisha  mazingira yanayozunguka makazi ya nyumba ili kuepuka ugonjwa wa maralia”alisema Kabeho.

Kiongozi wa mbio za mwenge wa uhuru kitaifa Charles Kabeho  alitowa wito huo baada ya kupokea taarifa hiyo kutoka kwa Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bukombe Dk Irene Mkerebe  wakati akitoa taarifa kwa kiongozi wa mbio za mwenge kitaifa walipokuwa wakifanya zoezi la ugawaji wa vyandarua kwa baadhi ya Wamama wajawazito na wanao nyonyesha kwenye  Zahanati ya Kijiji cha Iyogeyo Kata ya Iyogelo Wilayani Bukombe.
Dk Mkerebe alisema mwitikio wa wananchi uko chini  kutokana na wanaume kuto tumia vyandarua kitandani kwa madai kuwa vina maliza nguvu za kiume kuzalisha wadudu aina ya kunguni.
Dk Mkerebe alisema lakini wananchi wamekuwa wakishirikishwa kwa kupewa Elimu ya kutumia vyandarua na  tayali wamegawa kuanzia februari 2017 hadi februari 2018 vyandarua  26,357 kwa wanafunzi wa shule za msingi,  204,744 kwa akinama wajawazito na vyandarua 11,005 vimegawiwa kwa watoto wanao ugua surua na vyandarua `170,225 kwa wananchi ikiwa ni  lengo la kutekeleza mikakati ya kupambana na mbu waenezao maralia,kutoa Elimu dhidi ya maralia, ufatiliaji wa mabadiliko ya hali ya hewa ya mbu waenezao maralia kwenye vijiji viwili vinavyo vinaongoza kwa mbu wengi ambavyo ni Sinamila Kata ya Nganzo na Kijiji cha Imalamagigo Kata ya Igulwa.

Mkuu  wa Wilaya ya Bukombe Josephat Maganga wakati akipokea mwenge wa uhuru na kuzungumuza kwa niamba ya wananchi wa Wilaya ya Bukombe  katika viwanja vya Ofisi ya Kata ya Bugelenga alisema Mwenge wa Uhuru katika Wilaya ya Bukombe utakimbizwa  kilomita 123 na kupitia miradi ya maendeleo 8  mmoja wa kuwekewa jiwe la msingi,  mwingine mmoja wa kufunguliwa, miradi miwili ya kuzinduwa,  miradi mingine minne ya kuona na kufunguliwa yenye thamani ya Sh1,154,811,623.40.
Pia Mkimbiza Mwenge wa Uhuru Kitaifa Kabeho akihutubia wakazi wa kata ya Uyovu ulipo lala mwenge aliwakumbusha wananchi,wazazi na walezi kuwekeza watoto wao kwenye Elimu na kuwalea watoto kwenye misingi ya maadili mazuri na kuwanusulu vijana katika utumiaji wa madawa ya kulevya huku akisisitiza kupigana na adui wa haki, Rushwa kwa kutoa taarifa TAKUKURU wakati wananchi wanatafuta huduma kwenye ofisi yeyote na kuombwa rushwa na kuepukana na maambukizi mapya ya UKIMWI.





Comments