Mwanadada aizunguka Afrika kwa pikipiki

Mwanadada wa kituruki amekuwa gumzo katika mitandao ya kijamii kutokana na kufanya kwake ziara kwa kutumia pikipiki barani Afrika.

Alianza safari hiyo miaka mitano iliyopita baada ya mama yake kufariki.

Gulcin Sogut,mdada mwenye miaka thelathini na kitu yupo mbioni kutimiza ndoto yake ya kulizuru bara zima la Afrika.

Amekuwa akitumia dola 55 tu kwa siku wakati wa safari zake.

Akiwa na mwenzake Ferry Schouten kutoka Ulaya,watalii hao kwa sasa wapo Ethiopea baada ya kuvuka mpaka wa Kenya.

Mwanadada huyo mpaka sasa anaonekana kuwa na furaha kubwa kuendelea kulizunguka bara la Afrika ukitoa changamatoto kama vile kuendesha wakati wa mvua au katika majangwa na milima

Comments