Mhe Biteko: Tushirikiane kwa pamoja kuhakikisha Watoto wetu hawatembei umbali mrefu kutafuta elimu


Wanafunzi wa Sekondari zaidi ya 300 Kata ya Busonzo Tarafa ya Siloka Wilaya ya Bukombe Mkoani Geita, wanalazimika kutembea umbali mrefu zaidi ya kilomita 18 kutokana na ukosefu wa shule ya sekondari kwenye Kata hiyo wanafunzi wamekuwa wakienda Kata jirani ya Uyovu hali ambayo imekuwa ikipelekea wanafunzi wengi kukata tamaa na kushindwa kuhitimu kidato cha Nne.                    

Mratibu Elimu Kata ya Busonzo Ramadhan Mngoi aliyasema hayo wakati wa ziara ya Mbunge Jimbo la Bukombe ambae pia ni Naibu Waziri wa Madini Doto Mashaka Biteko alipo kuwa kwenye ziara Kata ya Busonzo Aprili 2 mwaka huu kwa lengo la kujuwa changamoto zinazo pelekea wanafunzi kutembea umbali mrefu na mradi wa shule ya Busonzo sekondari kushindwa kukamilika tangu mwaka 2012.

Mngoi  alisema Kata ya Busonzo ina shule za msingi tano zinafaulisha wanafunzi kujiunga na sekondari kila mwaka lakini tangu 2012 hadi mwaka 2017 wanafunzi zaidi 300 wanatembea umbali mrefu kutoka kijiji cha Namparahala kata ya Busonzo  kwenda Kata jirani ya Uyovu kwenye shuleni ya Runzewe sekondari wanatembea kilomita zaidi ya 18 kati ya wanafunzi hao hutoka vijiji vya mbali zaidi.

Mngoi alisema kutokana na umbali huo wanafunzi wamekuwa wakifauru kujiunga na masomo ya kidato cha kwanza lakini wanashindwa kufikia ndoto zao za kumaliza kidato cha nne kutokana na wengi wao kukata tamaa kwa kutembea umbali mrefu.


Alisema mwaka 2018 pekee wanafunzi walio anza kidato cha kwanza kutoka Kata ya Busonzo kwenda Kata jirani ya Uyovu ni zaidi ya wanafunzi 122 wanatembea kwa mingu na wengine kwa baiskeli na wazazi wengi wamekuwa wakishindwa kuwapangishia vyumba karibu na shule ya Runzewe sekondari kwa kwa madai kuwa wanashindwa kumundu gharama za kuwahudumia kama sehemu ya familia hali ambayo inapelekea wanafunzi hao kukata tamaa huku walioanza kidato cha kwanza ni wanafunzi 122 wanahitimu kidato cha nne wanafunzi 30 wengi wao kuishia kuolewa  na kuowa na kufanya biashara.

Mngoi alisema shule ya Runzewe sekondari imeadikisha zaidi ya wanafunzi 500 wakati uwenzo wa shule hiyo ni mdogo iwapo shule ya Busonzo sekondari itakapo kamilika na kufunguliwa matarajio mwenzi Junu mwaka huu itasaidia kupunguza msongamano wa wanafunzi Runzewe sekondari na kwamba kuna madarasa 4 nyumba ya mwalimu  moja matundu 10 ya choo wanafunzi, matundu 2 ya choo cha walimu kuna ujenzi wa maabara vyumba vitatu.


Diwani wa Kata ya Busonzo ambae pia ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Bukombe Safari Nikas Mayala alisema ujenzi wa shule ya Busonzo Sekondari umegharimu  nguvu za wananchi Sh milioni 8 serikari sh milioni 13  lakini choo cha wanafunzi choo cha walimu nyumba ya mwalimu imegharimu kuazia vyumba vya madarasa ni sh milioni 57  aliwaomba wananchi kuendela kuchangia mali na nguvu zao kwenye miradi ya maendeleo.



Mayala aliwaomba wananchi kuwa tayali kuchangia miradi ya maendeleo wakati wa miradi inapo anzishwa ili kuondoa changamoto zinazo wakabili wananchi ili waondokane na kutembea umbali mrefu kutafuta huduma za afya na wanafunzi kufata Elimu kata jirani.

Mbunge wa Jimbo la Bukombe Doto Mashaka Biteko wakati wa ziara yake ya kuhamasisha maendeleo Kata ya Busonzo Aprili 2 mwaka huu ambapo zaidi ya miaka  mradi wa ujenzi wa shule ya Busonzo Sekondari umeshindikana kukamilika kutokana na wananchi kujikita kwenye mambo ya kisiasa na kutoa changia maendeleo.


Biteko akiwa kwenye mkutano wa hadhara akipokea taarifa ya utekelezaji wa mradi huku  aliiomba serikali na imetoa sh 40 milioni  kupitia mfuko wa P4R kuongeza nguvu kuhakikisha shule hiyo inafunguliwa na kuchagia tofari 10,000 za choma zenye thamani ya million moja na laki mbili ambazo alizielekeza kukamilisha ujenzi wa vyumba vya maabara vitatu ili wanafunzi waondokane na changamoto ya kutembea umbali mrefu kutafuta Elimu Kata jirani ya Uyovu.


Biteko aliwaomba wananchi kuvuja makundi ya kisasa na kuwaunga mkono viongozi ambao wamechaguliwa na wananchi kwa kupingiwa kura na wengine kuajiliwa na serikali pamoja na  kuwaelimisha wananchi madhara ya kuendekeza siasa wakati uchaguzi umekwisha hali ambayo inakwamisha maendeleo na kuwapa mzingo wananchi ambao wanahitaji kusogezewa huduma za kijamii.




Comments