WILAYA YA BUKOMBE YATOA CHANJO YA KUZUIA SARATANI YA MLANGO WA UZAZI KWA WASICHANA WENYE UMRI WA MIAKA 14
Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe Mkoani Geita,kwa
kushirikiana na Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia, Wazee na Watoto,
kupitia mpango wa chanjo ya kuzuia saratani ya mlango wa kizazi mwaka 2018/19
wasichana 2800 wenye umri wa miaka 14
watafikiwa kupewa chanjo hiyo ikiwa wengi wao ni wanafunzi shule za msingi na
sekondari pia chanjo itatolewa kwa wasichana ambao hawasomi kwa kushirikiana na
viongozi wa serikali za vijiji.
Aliyasema hayo Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bukombe Dk
Irene Bukerebe kwenye uzinduzi wa kiwilaya wa wiki ya Chanjo ya kuzuia sataratani
ya mlango wa kizazi kwenye viwanja vya Kituo cha Afya Ushirombo Kata ya Bulangwa
katika uzinduzi huo wasichana 124 wenye
umri wa miaka 14 walichanjwa chanjo hiyo ikiwa malengo ya halmashauri
hiyo nikuwafikia wasichana 2800 kwa mwaka 2018/19.
Dk Bukerebe alisema mwaka 2017 takwimu ya wanawake 1700 wenye
umri wa miaka 30 hadi 50 walihamasishwa kupima kwa hiyali saratani ya mlango wa kizazi katika hospitali ya Wilaya kati yao 147 walikutwa na dalili za ugonjwa
huo na waliazishiwa matibabu huku miongoni mwao wanawake 17 walikutwa na ugonjwa
wa saratani ya mlango wa kizazi, na kulazimika kupelekwa hospitali ya rufaa Bugando
Mwanza kwa matibabu zaidi.
Miongoni mwawanafunzi walio patiwa chanjo ya kuzuia saratani
ya mlango wa kizazi toka shule ya msingi Kapera darasa la saba Agnes Ezekiel
alisema chanjo hiyo itamsaidia kujikinga na magonjwa huku akiwaomba wanafunzi wezake
kuacha tabia ya kujiingiza kwenye dimbwi la mapenzi wakawa na umri mdogo.
Nae Diwani wa Kata ya Bulangwa Mhe. Yusuph Mohamed aliiomba serikali kuwachukulia hatua wazazi watakao bainika wamewakataza watoto wao kupatia chanjo kwa kuamini mila potofu hali ambayo huendeleza kuunda jamii ya wasiojitambua.
Nae Diwani wa Kata ya Bulangwa Mhe. Yusuph Mohamed aliiomba serikali kuwachukulia hatua wazazi watakao bainika wamewakataza watoto wao kupatia chanjo kwa kuamini mila potofu hali ambayo huendeleza kuunda jamii ya wasiojitambua.
Mkuu wa Wilaya ya Bukombe Josephat Maganga akiwahutubia
wananchi katika uzinduzi huo aliwaomba wazazi na walezi kuachana na mila potofu
kwenye chanjo zinazotolewa na serikali kupitia watalamu wa Afya badalayake wazazi
wawaruhusu watoto wao wakapewe chanjo ya ugonjwa huo ili wasije wakakubwa na
ugonjwa wa saratani ya mlango wa kizazi, au vifo visivyo vya lazima.
Aliagiza serikali za vijiji kuzitambua kaya zenye wasichana
wenye umri wa miaka 14 ambao hawasomi ili nao wapatiwe chanjo mara tu watalamu wa afya watakopo
kuwa wanapita kutoa huduma ya chanjo ya kuzuia saratani ya mlango wa kizazi mashuleni na vijijini kwenye
ofisi za serikali, "lengo la serikali nikukinga magonjwa na kuwa na taifa lenye
wanawake bora wenye uwezo wa kufanya kazi za uzalishaji mali kuanzia ngazi ya
familia hadi taifa."Maganga alisema
Pia Maganga alitowa wito kwa wanasichana wenye umri wa miaka 9 na
14 kutojihusisha na mapenzi wakawa wa umri mdogo na kuwasisitiza kuwa ni chanzo cha kupata ugonjwa
wa saratani ya mlango wa kizazi huku akiwaomba wazazi na walezi kuwaelimisha watoto
wao ili wazingatie maadili ili kuepukana na maradhi pamoja na mimba za utotoni zinazojitokeza mara kwa mara katika jamii.
Comments
Post a Comment