RAIS MAGUFULI ANA MAKUSUDI MAKUBWA NA WATANZANIA, TUMUOMBEE

Naibu Waziri wa Madini ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe Doto Mashaka Biteko akiwasitiza waumini waliohudhiria kwenye ibada ya jumapili katika kanisa la EAGT lililopo katika kijiji cha Dyobahika, Kata ya Uyovu, Wilayani Bukombe Leo 4 Machi 2018 wakati akitoa salamu za serikali. 
Mbele ya waumini wa kanisa la EAGT lililopo katika kijiji cha Dyobahika, Kata ya Uyovu, Wilayani Bukombe, Naibu Waziri wa Madini ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe Doto Mashaka Biteko akiwasihi waumini waliohudhiria kwenye ibada ya jumapili kuunga mkono juhudi za serikali ya awamu ya tano,  Leo 4 Machi 2018.
Naibu Waziri wa Madini ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe Doto Mashaka Biteko (Kulia), Katibu wa Mbunge huyo katika jimbo la Bukombe Elius Benjamin Mgeta (Katikati), na Katibu wa Naibu Waziri huyo Mhandisi Kunguru Kasongi  wakifatilia mahubiri katika kanisa la EAGT lililopo katika kijiji cha Dyobahika, Kata ya Uyovu, Wilayani Bukombe, Leo 4 Machi 2018.
Mbele ya waumini wa kanisa la EAGT lililopo katika kijiji cha Dyobahika, Kata ya Uyovu, Wilayani Bukombe, Naibu Waziri wa Madini ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe Doto Mashaka Biteko akiwasihi waumini waliohudhiria kwenye ibada ya jumapili kuunga mkono juhudi za serikali ya awamu ya tano,  Leo 4 Machi 2018.


Ni miaka miwili sasa na ushee imepita tangu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt John Pombe Magufuli aingie madarakani tarehe 5 Novemba mwaka 2015, ambapo mpaka sasa kuna mambo mengi ameyafanya ambayo ni moja ya sehemu za ahadi zake alizoahidi alipokuwa akiinadi ilani ya Chama Cha Mapinduzi kwenye kampeni za uchaguzi mkuu mwaka 2015.
Miongoni mwa mambo msingi kabisa katika serikali ya awamu ya tano ni pamoja na uwajibikaji wa watumishi wa umma na wananchi kwa ujumla kwani kumekuwepo na ari ya kufanya kazi kwa bidii na weledi mkubwa, umakini wa wananchi katika ulipaji wa kodi, vita ya ufisadi imekuwa kubwa na imesaidia kuleta mageuzi na fedha ambazo zimekuwa zikiokolewa kutokana na vita hiyo zinaelekezwa kwa wananchi kupitia miradi ya maendeleo,  Kuongezeka maradufu kwa ukusanyaji wa mapato kutoka Sh 9.9 trilioni kwa mwaka hadi Sh14 trilioni kwa mwaka.
Naibu Waziri wa Madini ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe Doto Mashaka Biteko amebainisha hayo Leo 4 Machi 2018 wakati akitoa salamu za serikali kwenye ibada ya jumapili katika kanisa la EAGT lililopo katika kijiji cha Dyobahika, Kata ya Uyovu, Wilayani Bukombe.
Mbele ya waumini hao Mhe Biteko alisema kuwa mambo mengine muhimu yaliyofanywa na Rais Magufuli ni pamoja na utekelezaji wa miradi mikubwa kama vile ujenzi wa reli ya kisasa na uboreshaji wa shirika la ndegeKatika sekta ya kilimo serikali ya Rais Magufuli imeondoa Tozo na Kodi nyingi zilizokuwa kero kwa watanzania ikiwa ni pamoja na elimu  bure kuanzia ngazi ya shule ya awali mpaka sekondari.
Aliongeza kuwa serikali inapigania kwa makusudi makubwa kabisa rasilimali za Taifa, ambapo vita katika eneo la madini ilipelekea kupitia upya mikataba yote ya uwekezaji jambo ambalo limefanya kujitambua kama Taifa lenye rasilimali nyingi na muhimu hatimaye sasa wawekezaji wanajua Tanzania ukienda lazima uheshimu sheria na taratibu za nchi katika uwekezaji na uchimbaji wa madini.
Biteko alisema katika miaka ya nyuma wawekezaji wa kigeni walitumia vibaya rasilimali za Taifa ambapo katika sekta ya Madini walichimba Madini mbalimbali nchini pasina kunufaisha watanzania waliondoka nayo na kunufaisha mataifa watokayo.
Aliwaeleza waumini hao kuwa jukumu lao kuu kwa sasa ni kuiamini serikali inayoongozwa na Rais Magufuli lakini jambo la pili ni kuiombea serikali nzima ili kutimiza wajibu wake kwa watanzania kwa haki pasina upendeleo.
"Ndugu zangu naomba niwaambie ukweli kabisa kuna watu wanasema hawamuelewi Rais wetu, yawezekana haeleweki kwa kuwa anasimamia haki kwa ajili ya wananchi wanyonge na kuwatoa katika maisha ya mazoea waliyoishi katika kipindi kirefu na kuyageuza ndio utaratibu" Alikaririwa Biteko (Mb) huku akishangiliwa na mamia ya waumini hao
Katika hatua nyingine Mhe Biteko amekemea vikali siasa zinazorudisha nyuma maendeleo badala yake amewataka wanasiasa wenzake kuhubiri kweli na siasa yenye tija ya maendeleo kwa wananchi.

Comments