NAIBU WAZIRI WA MADINI AWAHIMIZA WAUMINI WA MADHEHEBU YA DINI KUCHANGIA MAENDELEO


 Wanakwaya wa Kanisa la Wadventista Wasabato Maganzo wakitoa mahubiri kwa njia ya nyimbo.
 Waumini
Diwani wa Kata ya Ushirombo Mhe. Lameck Warangi ambae pia ni muumini wa Kanisa hilo akizungumza na Waumini wenzake

 Naibu wa Waziri wa Madini ambae pia ni Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe. Doto Mashaka Biteko akiwa amejumuika na viongozi pamoja na waumuni wa Kanisa la Wadventisti Wasabato- Maganzo kuwaombea viongozi wa serikali ya awamu ya tano waendelee kuchapa kazi.



Waumini wa madhehebu mbali mbali ya kidini wametakiwa kuendelea kuchangia maaendeleo ya kanisa na miradi ya maendeleo inayoibuliwa kwenye vijiji wanako toka.
Rai hiyo ilitolewa na  Naibu waziri wa madini  pia Mbunge wa Jimbo la Bukombe Doto Mashaka Biteko wakati akijibu risala  ililohitaji mchango wa Tsh  milioni 10 kwa ajili ya ununuzi wa vyombo vya mziki  vya kisasa vya kanisa la Waadventista Wasabato Maganzo  Wilaya ya Bukombe  Mkoani  Geita.

Biteko alichangia Tsh milioni mbili hali ambayo ilipelekea Mbunge kuendesha harambe kanisani hapo na kukusanya fedha milioni 4.6  ambapo keshi ilipatika Tsh milioni mbili huku zingine zikitolewa  ahadi za viongozi wa kanisa hilo.

Awali mwenyekiti wa kinamama kanisani hapo Savera Mandago alisema kuwa waumini wa kanisa hilo wanafuraha ya kuabudu pamoja na Naibu Waziri wa Madini pia Mbunge wao nakwamba kanisa la Maganzo nikituo kikuu cha Makanisa ya Wasabato Wilaya ya Bukombe jumla ya washirika waumini 918  kutokana na changamoto ambayo wamekuwa wakiipata wakati wa makambi wanakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa vyombo vya mziki.
Mandago kupitia risala alimuomba Naibu Waziri wa madini kuchangia TSh  milioni 10 ili wanunuwe vyombo vya mziki wa kisasa ambao utawarahisishia kuendeleza kazi ya Mungu.
Mkurugenzi wa shule ya Emink sekondari  Emmanuel Kalamu akiahidi Sh 700,000 aliutupia lawama uongozi wa kanisa hilo katika mwaliko wake hakuadaliwa kuwa kutakuwa na changizo hali ambayo agejianda vizuri badara ya kiasi hicho alicho tamuka.
Mchungaji wa kanisa la Waadventista Wasabato Maganzo  Mch. Godwin Lazaro akishukuru wageni waalikwa na kuchangia mali zao kuwezesha kazi ya Mungu alisema wataendelea kumuunga mkono Naibu Waziri wa Madini kwenye Jimbo la Bukombe katika kuchangia shughuli za maendeleo nje ya kanisa na kanisani ili kufikia malengo.

Comments