Mhe Biteko awatoa hofu wafugaji Jimboni kwake


Naibu Waziri wa Madini ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mkoani Geita Mhe. Doto Mashaka Biteko amekutana na wafugaji wa Kata ya Iyogelo na kuzungumza nao huku akiwasisitiza wazingatie agizo la serikali kuondoa ng’ombe ndani ya hifadhi ya kigosi Muyowosi na kuanzisha ufugaji wa kisasa
 
Biteko alitoa tamko hilo wakati akizungumuza na wafugaji wa ng’ombe kata ya Iyogelo walipo muomba aishawishi serikali kuwakatia sehemu ya marisho kwenye pori la akiba linalo pakana na Wilaya ya Bukombe.
Naibu Waziri wa Madini Biteko wakati wa ziara yake ya kwenda anasikiliza kero za wananchi Jimboni kwake, wafugaji amewambia kuwa hawezi kwenda kushawishi serikali kuvuja sheria ya kuhifadhi mapori ya akiba nchini yaliyo tengwa kisheria na kuwasihi nao wahusike  kuitunza lasilimali ya taifa kwa faida ya vizazi vijavyo.
“nilichokiona kwa wafugaji wa Kata ya Iyogelo wanataka marisho, na kuna manyanyaso kati ya askari wa wanyamapori na wafugaji,pia  wafugaji wenyewe kwa wenyewe kugeukana na kucholeana dili kwa askari wa wanyamapori, kibaya zaidi wananchi wakawaida kujifanya askari wa wanyama pori  swala la pori kukatwa kwa ajili ya marisho haitawezekana kwa sasa lakini  wananchi naomba kueni na uvumilivu “alisema Biteko.
Alisema serikali inajipanga kutatua kero za wafugaji ndio maana imeelekeza ngombe wa watanzania wapigwe chapa na kuwaomba wafugaji kubadilika kulingana na mabadiliko ya nyakati viongozi wa serikali zilizopita hawakusimamia sheria ndio maana wafugaji hao walijijengea tabia ya kuchungia mifugo ndani ya hifadhi na kuongeza kuwa  asilimia 80 ya ardhi Wilaya ya Bukombe ni hifadhi asilimia 20 ni kwa ajili ya makazi, kilimo, na shughuli mbali mbali za kibinadamu.
Biteko aliwaomba wafugaji kupunguza mifungo yao badara ya kuwa na ng’ombe 1000 wauze wabakize 10 na wazifuge kisasa ili kwendana na maelekezo ya serikali na kuacha tabia ya kuomba serikali kukata pori kwa ajili ya marisho.

Miongoni mwa wafugaji Luziri Abeli alimuomba Naibu Naziri wa Madini kuwa afatilie ahadi ya Rais John Magufuli wakati wa kampeni yake 2015 kuwa wampigie kura atawategea maeneo ya marisho hoja hiyo iliungwa mkono na mfugaji Lucas Elias nakuongeza kuwa serikali ione umuhimu wa kutenga eneo ndani ya hifadhi wafugaji wako tayali kulipia kila mwezi hali ambayo itaongeza pato la taifa.
 
Ofisa mifungo Kata ya Iyogelo Aroyce Mbulamatale alimpongeza Naibu Waziri wa Madini ambae ni Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe. Doto Mashaka Biteko kwa kusimamia sheria za nchi na kwamba Kata ya Iyogelo inang’ombe 5.017 na tayali wamepigwa chapa kufuatia angizo la serikali ili kutambua mifungo ya wafugaji wa kitanzania ili serikali itowe huduma kwa wananchi jamii ya wafugaji na kuwasihi wananchi hao kuwa na subira wakati serikali ikifanya mchakato wa kuwatengea maeneo kuliko kuvunja sheria kwa kuwapoleka mifugo tena katika pori la akiba na kujikuta wanawajibishwa kisheria ikiwemo kufirisiwa mifugo yao.


Comments